-
Nigeria: Kifo cha kiongozi wa Boko Haram kimethibitishwa bila shaka yoyote
Jun 17, 2021 08:02Kifo cha aliyekuwa kiongozi wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la wanamgambo wa Boko Haram wenye makao yao nchini Nigeria kimethibitishwa pasina shaka yoyote. Taarifa hiyo imetolewa kupitia tangazo kwa njia ya video lililotolewa na kiongozi mpya wa Boko Haram, Bakura Modu.
-
Kero la ugaidi; 50 wauawa Burkina Faso na Nigeria
Jun 15, 2021 22:05Jeshi la Burkina Faso limetangaza kuwa magaidi 25 wameuliwa katika operesheni iliyofanywa na askari wa jeshi hilo.
-
Polisi ya Nigeria yafyatua gesi ya kutoa machozi katika maadhimisho ya Siku ya Demokrasia
Jun 12, 2021 22:20Polisi wa Nigeria wamefyatua gesi ya kutoa machozi kutawanya waandamanaji wanaopinga serikali huko Lagos na katika mji mkuu, Abuja, na ripoti zinasema kuwa baadhi ya wanaadamanaji hao wakamatwa na wengine kujeruhiwa.
-
Wanakijiji 90 wauawa katika shambulio la wabeba silaha Nigeria
Jun 12, 2021 08:13Watu wasiopungua 90 wameuawa baada ya genge la watu waliojizatiti kwa silaha kushambulia kijiji kimoja huko Kaskazini Magharibi mwa Nigeria.
-
Wiki ya Imam Khomeini yaadhimishwa nchini Nigeria
Jun 07, 2021 22:22Wanafunzi Waislamu wa Vyuo Vikuu na taasisi za elimu ya juu za Nigeria wameandaa Wiki ya Imam Ruhullah Khomeini, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, katika jimbo la Bauchi, kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Jumuiya za kimataifa zalaani hatua ya Nigeria ya kuifungia Twitter
Jun 07, 2021 03:32Jumuiya za kimataifa na balozi za nchi za kigeni nchini Nigeria zimelaani hatua ya serikali ya nchi hiyo ya kuufungia mtandao wa kijamii wa Twitter kwa muda usiojuliikana.
-
Serikali ya Nigeria yaufungia mtandao wa Twitter kwa muda usiojulikana
Jun 05, 2021 07:12Serikali ya Nigeria imetangaza kuwa, hatua ya mtandao wa kijamii wa Twitter ya kuufuta ujumbe mmoja wa Rais Muhammadu Buhari wa nchi hiyo haikubaliki kabisa hivyo Abuja ameamua kuufungia mtandao huo kwa muda usiojulikana. Twitter kwa upande wake imesema inafuatilia kwa kina suala hilo.
-
Jeshi la Nigeria laangamiza magaidi 50 wa Boko Haram
Jun 03, 2021 22:15Jeshi la Nigeria limetangaza habari ya kuangamiza magaidi wasiopungua 50 wa kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Familia za wanafunzi waliotekwa nyara Nigeria zaitaka serikali kuwakomboa
Jun 02, 2021 07:02Familia za wanafunzi waliotekwa nyara na magenge ya wahalifu nchini Nigeria na vilevile jumuiya za kimataifa za kutetea haki za binadamu zimeitaka serikali ya Nigeria kuchukua hatua madhubuti za kukomboa karibu wanafunzi 200 wa shule moja ya Kiislamu waliotekwa nyara na magenge ya wahalifu katikati mwa Nigeria.
-
Kuendelea harakati za magaidi nchini Nigeria; wanafunzi 200 watekwa nyara
Jun 01, 2021 21:58Makundi ya kigaidi katika eneo la Afrika Magharibi hasa nchini Nigeria yamekithirisha vitendo vya uhalifu, na katika tukio la hivi karibuni wanafunzi karibu 200 wa shule moja ya Kiislamu wametekwa nyara kati mwa Nigeria.