-
Katibu Mkuu wa UN alaani hujuma dhidi ya shule Nigeria
Dec 15, 2020 23:42Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali hujuma iliyofanywa Ijumaa iliyopita katika shule ya sekondari mkoani Katsina nchini Nigeria, ambapo mamia ya wavulana walitekwa nyara na wahalifu waliokuwa na silaha.
-
Msomi wa Nigeria: Sheikh Ibrahim Zakzaky anashikiliwa kizuizini kwa amri ya Saudi Arabia
Dec 13, 2020 23:25Sheikh Abdul-Hamid Bilo, mmoja wa wanazuoni wa Kishia nchini Nigeria amesema kuwa, Sheikh Ibrahm Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria anashikiliwa kizuizini kwa amri ya watawala wa Kiwahabi wa Saudi Arabia.
-
Kumbukumbu ya mauaji ya Waislamu huko, Zaria kaskazini mwa Nigeria
Dec 12, 2020 03:56Leo Waislamu wa Nigeria wanakumbuka mauaji yaliyotekelezwa na jeshi la nchi hiyo katika mji wa Zaria jimboni Kaduna, dhidi ya wanachama wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria.
-
ICC: Tuna ushahidi wa kutosha wa kuwafungulia mashtaka maafisa wa Nigeria
Dec 11, 2020 23:58Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, ICC, amesema kuwa, ana ushahidi wa kutosha wa kuweza kuwafungulia mashtaka maafisa wa Nigeria kuhusu mateso na ukandamizaji waliofanyiwa wananchi wa nchi hiyo.
-
Nigeria inatumia vifaa vya kijasusi vya Israel dhidi ya wapinzani
Dec 09, 2020 08:28Ripoti mpya imefichua kuwa, Shirika la Kijasisi la Jeshi la Nigeria (DIA) linatumia programu ya kijasusi ya Israel kudukua na kupeleleza simu na jumbe fupi za simu za wapinzani na raia wengine nchini humo.
-
Serikali ya Nigeria inatumia vibaya programu za ujasusi za Wazayuni dhidi ya raia wa nchi hiyo
Dec 09, 2020 04:10Ripoti iliyotolewa na Chuo Kikuu kimoja cha nchini Canada imeeleza kuwa, serikali ya Nigeria inatumia vibaya programu za utawala wa Kizayuni kufuatilia maongezi na jumbe za wapinzani na raia wengine wa nchi hiyo.
-
Jinai mpya ya Boko Haram, muendelezo wa misimamo ya kufurutu ada Afrika
Nov 30, 2020 09:44Baada ya makundi ya kigaidi kudhoofishwa katika maeneo mbali mbali ya Asia Magharibi, hivi sasa makundi hayo yameeneza satwa yao na kuimarika katika maeneo mbali ya barani Afrika ambapo yamekithirisha hujuma. Katika tukio la hivi karibuni, magaidi wakufurishaji wa Boko Haram wameua wakulima 110 katika kijiji cha Koshobe karibu na Maiduguri, mji mkuu wa jimbo la Borno ambalo ni kitovu cha magaidi hao, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Kuendelea malalamiko ya Wanigeria katika kumtetea Sheikh Zakzaki
Nov 26, 2020 06:14Katika kuendelea kushikiliwa kinyume cha sheria Sheikh Ibrahim Zakzaki, Kiongozi wa Waislamu wa Nigeria, Waislamu wa nchi hiyo kwa mara nyingine tena wamefanya maandamano makubwa ya kuunga mkono na kutaka mwanzuoni huyo wa Kiislamu aachiliwe mara moja.
-
Boko Haram yatungua helikopta Nigeria na kuua watu 5
Nov 19, 2020 03:25Kundi la kigaidi la Boko Haram limetungua ndege aina ya helikopta huko kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuua watu watano.
-
Wananchi wa Nigeria watoa ushahidi kuhusu jinai za jeshi la nchi hiyo
Nov 15, 2020 23:05Kamati ya Mahakama ya Nigeria imeripoti kuwa, raia wa nchi hiyo wamewasilisha ushahidi wao wa kimaandishi kuhusu jinai na uhalifu uliofanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya raia.