-
Mwanachama mwingine mwandamizi wa HAMAS amewekwa kizuizini nchini Saudi Arabia
Sep 17, 2019 03:42Duru za Palestina zimetangaza kuwa mwanachama mwingine mwandamizi na muhimu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amekamatwa na kuwekwa kizuizini nchini Saudi Arabia.
-
Iran: Uchu wa madaraka wa 'Hitler mdogo' chachu ya kuangamizwa mapema Israel
Sep 15, 2019 03:19Msaidizi Maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amemtaja Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, kama 'Hitler mdogo' na kusisitiza kuwa uchu wa madaraka wa Benjamin Netanyahu utakuwa mwanzo wa kuporomoka na kusambaratika utawala huo haramu.
-
Wanamuqawama wa Palestina watungua drone ya Israel Ukanda wa Gaza
Sep 14, 2019 23:06Vikosi vya muqawama vya Palestina vimefanikiwa kutungua ndege isiyo na rubani ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Qatar: Palestina ni kadhia muhimu zaidi ya nchi za Kiislamu na Kiarabu
Sep 12, 2019 07:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amelaani hatua ya Wazayuni kukiuka haki za taifa la Palestina na kusema: "Palestina ni kipaumbele cha kwanza kwa nchi za Kiislamu na Kiarabu."
-
Malengo ya safari ya waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni huko Al Khalil
Sep 06, 2019 01:34Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Utawala wa Kizayuni wa Israel Septemba Nne, kwa mara ya kwanza alifika katika mji wa Al Khalil (Hebron) katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kisha akaingia katika msikiti maarufu wa Masjid Ibrahimi katika mji huo. Kabla ya safari hiyo ya Netanyahu, rais wa utawala wa Kizayuni Reuven Rivlin naye pia alifika katika mji wa Al Khalil na kutembelea Masjid Ibrahimi.
-
Makumi ya Wapalestina wajeruhiwa kwa risasi katika maandamano ya "Haki ya Kurejea"
Aug 31, 2019 03:12Makumi ya Wapalestina wamejeruhiwa kwa risasi katika Ijumaa ya 72 ya maandamano ya 'Haki ya Kurejea' yaliyofanyika kwa kaulimbiu ya "Utiifu kwa Mashahidi.
-
Mahmoud Abbas: Marekani haisaidii juhudi za kurejesha amani Mashariki ya Kati
Aug 30, 2019 22:14Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa Marekani haisaidii juhudi za kurejesha amani na usalama katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Makampuni ya Imarati yanunua ardhi za mji wa Quds kwa ajili ya Wazayuni
Aug 29, 2019 03:22Naibu Mwenyekiti wa Harakati ya Kiislamu ya Palestina amesema kuwa makampuni ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) yananunua ardhi huko Quds na kisha kukabidhi umiliki wa ardhi hizo kwa Waisraeli.
-
Arab League: Uamuzi wa Marekani wa kulifuta jina la Palestina ni kitendo cha "uadui"
Aug 28, 2019 22:07Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) imesema, uamuzi mpya uliochukuliwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani wa kulifuta jina la Palestina katika orodha ya maeneo ya Magharibi ya Asia ni kitendo cha "uadui".
-
Marekani yafuta jina la Palestina katika orodha ya nchi za dunia
Aug 26, 2019 08:25Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imechukua hatua isiyo ya kawaida kwa kufuta jina la Palestina katika orodha ya nchi na maeneo mbalimbali ya dunia.