-
Mhadhiri Ghana: Kimya cha dunia kwa jinai za Israel Gaza kinaaibisha
Apr 14, 2025 13:29Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Ghana,Mustapha Abdullah Kuyateh amelaani vikali hujuma za kikatili za Israel dhidi ya Gaza, akisisitiza kuwa huo ni mwendelezo wa mauaji ya kimbari na mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina.
-
Polisi ya Uholanzi yakandamiza maandamano ya kuitetea Palestina
Apr 12, 2025 11:39Makabiliano yaliripuka mjini Amsterdam kati ya polisi ya Uholanzi na waandamanaji wanaoiunga mkono Palestina, wakati waandamanaji hao wakipita katika kitovu cha fedha cha mji huo, wakizituhumu kampuni kubwa kwa kujinufaisha kutokana na uhusiano wao na Israel wakati huu wa vita vinavyoendelea Gaza.
-
Mgawanyiko katika jeshi la Israel huku mashambulio dhidi ya Gaza yakiendelea
Apr 11, 2025 02:03Kundi la askari wa akiba wa jeshi la anga la Israel limefukuzwa kazi baada ya kutia saini waraka wa kutaka kusitishwa vita dhidi ya Gaza na kurejeshwa kwa mateka wa utawala huo haramu.
-
Wapalestina wengine 40 wauawa shahidi Gaza na mabomu ya Wazayuni
Apr 10, 2025 02:54Utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kumwaga damu za Wapalestina; ambapo umewauwa Wapalestina karibu 40 wakiwemo watoto katika mashambulizi ya anga ya karibuni katika maeneo kadhaa katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
-
Maelfu ya Wamisri waandamana Sinai kuiunga mkono Palestina
Apr 09, 2025 13:42Maelfu ya wananchi wa Misri kutoka majimbo mbalimbali wamekusanyika karibu na Uwanja wa Ndege wa El-Arish katika Mkoa wa Sinai Kaskazini wakitangaza kuunga mkono kadhia ya Palestina na kupinga jaribio lolote la kuwafurusha Wapalestina kutoka katika ardhi zao.
-
Israel 'yaumbuka' baada ya vidio kufichua ukweli halisi kuhusu mauaji ya wahudumu 15 wa tiba
Apr 06, 2025 06:45Vidio iliyopatikana kwenye simu ya mfanyakazi wa Kipalestina wa huduma za tiba aliyeuawa shahidi pamoja na wenzake 14 huko Ghaza mwezi uliopita, inasuta na kukinzana na madai yaliyotolewa na jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kuhusu namna mauaji ya wahudumu hao yalivyotokea.
-
Wanazuoni wa Kiislamu watoa fatwa; Mataifa ya Kiislamu yaunge mkono Muqawama wa Palestina
Apr 05, 2025 07:19Umoja wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (IUMS) umetoa fatwa (agizo la kidini) ukizitaka nchi za Kiislamu kutoa msaada wa haraka wa kijeshi, kifedha na silaha kwa mrengo wa Muqawama wa Palestina, ili kukabiliana na mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala katili wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
SEPAH: Muqawama utakomesha uwepo mchafu wa utawala wa Kizayuni
Apr 04, 2025 03:14Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la nchini Iran SEPAH limetoa taarifa na kutangaza kuwa: "Kambi ya Muqawama hususan wanamapambano shupavu na mashujaa wa Palestina hatimaye itamaliza na kuyakatisha maisha ya aibu ya wavamizi wa Palestina."
-
Pezeshkian: Mataifa ya Kiislamu yanaweza kukomesha jinai za Israel
Apr 03, 2025 11:38Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema umoja na mshikamano miongoni mwa mataifa ya Kiislamu unaweza kuwa chachu ya kukomeshwa jinai za kuogofya za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yaua Wapalestina wengine karibu 80 Gaza, Guterres asikitika
Apr 03, 2025 07:05Makumi ya Wapalestina wengine wameuawa shahidi katika mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza usiku kucha.