Hamas: Muqawama utaendelea kukabiliana na mashambulizi ya Israel
-
Usama Hamdan
Afisa wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameonya kuwa kuendelea mashambulizi na hujuma za Israel kunazidisha mapambano na muqawama wa wananchi wa Palestina dhidi ya maghasibu Wazayuni.
Usama Hamdan ambaye ni mmoja wa maafisa wa ngazi ya juu wa Hamas amesema: Tangu wiki nne zilizopita hadi sasa serikali ya Marekani haijatangaza msimamo wowote wa wazi wa kulaani hatua ya Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, ya kukataa pendekezo la kusimamisha vita.
Afisa huyo wa ngazi ya juu wa Hamas amesisitiza kuwa katika muda huu wote hakuna ishara yoyote mpya kutoka kwa Wazayuni maghasibu ya kusitisha mashambulizi katika maeneo ya Palestina.
Hamdan ameongeza kusema: Hamas inaendeleza jitihada za kufikiwa mapatano ya kusitisha vita na mashambulizi dhidi ya watu wa Palestina.
Ameshiria pia kwamba Hamas pamoja na wapatanishi wanafanya juhudi za kufikiwa usitishaji vita na kufunguliwa vivuko ili kuruhusu misaada na kuboresha hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.