-
Hizbullah: Iran ndiye muungaji mkono mkuu wa kadhia ya Palestina
Mar 30, 2025 07:21Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza nafasi muhimu ya Iran katika kuunga mkono kadhia ya Palestina ya kukombolewa kuondokana na uchokozi na uvamizi wa Israel huku akiulaani vikali utawala wa Israel kwa ukatili wake katika eneo zima ambao unawezeshwa kwa kiasi kikubwa na uungaji mkono wa Marekani.
-
Wanachuo 300 wapokonywa viza US kwa kuiunga mkono Palestina
Mar 30, 2025 06:29Marekani imebatilisha viza za wanafunzi zaidi ya 300 wa kigeni kwa kuratibu na kushiriki katika maandamano ya kuwanga mkono na kuwatetea wananchi madhulumu wa Palestina katika mabewa ya vyuo vikuu kote nchini humo.
-
Jeshi la Israel lamuua Msemaji wa HAMAS katika muendelezo wa mauaji ya kimbari Ghaza
Mar 27, 2025 05:57Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limemuua shahidi Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Abdel-Latif al-Qanoua, katika shambulio la kigaidi usiku wa manane wa kuamkia leo lililolenga eneo la Jabalia kaskazini, katika Ukanda wa Ghaza.
-
Tunisia yalaaniwa kwa kumkamata mwanachuo aliyepeperusha bendera ya Palestina
Mar 26, 2025 11:12Mwanafunzi mmoja wa Tunisia amekamatwa kwa kuingia uwanjani na kupeperusha bendera ya Palestina wakati wa mechi ya kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026 katika mji mkuu wa nchi hiyo, Tunis.
-
Mtengeneza filamu mashuhuri ya Palestina iliyoshinda Oscar apigwa na kukamatwa na askari wa Israel
Mar 25, 2025 11:47Hamdan Ballal, mtengeneza filamu mwenza wa Kipalestina wa filamu iliyoshinda tuzo ya Oscar iitwayo Hakuna Ardhi Nyingine (No Other Land) amekamatwa na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya sana na walowezi wa Kizayuni. Hayo yameripotiwa na Yuval Abraham aliyeshirikiana naye kutengeneza filamu hiyo.
-
Jeshi katili la Israel laendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza
Mar 25, 2025 02:51Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina wengine 17 katika mashambulizi ya alfajiri ya leo katika Ukanda wa Gaza, siku moja baada ya kuua shahidi Wapalestina zaidi ya 60 akiwemo ripota wa Al Jazeera, Hossam Shabat katika ukanda huo.
-
Siku ya saba ya uvamizi wa Israel wa Ghaza; makumi wauawa na kujeruhiwa
Mar 24, 2025 10:51Utawala wa wa Kizayuni wa Israel Israel unaendelea kufanya jinai na mashambulizi ya anga katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ghaza ambapo tangu asubuhi ya leo hadi wakati tunaandaa taarifa hii, makumi ya Wapalestina wamekuwa wameshauwa shahidi na kujeruhiwa, leo ikiwa ni siku ya saba ya tangu kuanza wimbi jipya la jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza.
-
Israel yapigwa na makombora kutoka Yemen, ving'ora vyahanikiza
Mar 23, 2025 10:51Vikosi vya Ulinzi vya Yemen vimevurumisha makombora kuelekea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel, na kuwatia kiwewe na hofu Wazayuni; huku safari za ndege zikisimamishwa Tel Aviv.
-
Rais wa Mexico ampokea rasmi balozi mpya wa Palestina
Mar 23, 2025 02:47Rais wa Mexico, Claudia Sheinbaum amepokea rasmi hati za utambulisho za Balozi wa Palestina Nadya R. H. Rasheed katika Ikulu ya Mexico City.
-
Netanyahu: Mashambulio yalioua watoto 174 Gaza ni mwanzo tu
Mar 20, 2025 03:10Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ametangaza kushadidi mashambulio mabaya dhidi ya Gaza, akionya kwamba mashambulizi ya hivi karibuni ya anga, ambayo yaliua watoto wasiopungua 174 katika ukanda huo, ni mwanzo tu wa uchokozi mkubwa zaidi dhidi ya Wapalestina.