-
Wanajeshi wa Israel wameua watoto 54 Wapalestina
Dec 20, 2018 01:13Wanajeshi wa utawala haramu wa Israel wameua watoto 54 Wapalestina katika mwaka huu wa 2018 unaomalizika.
-
Palestina yazitaka nchi za Kiarabu na Kiislamu zikate uhusiano wao na Australia
Dec 19, 2018 11:47Mamlaka ya Ndani ya Palestina imekataa msaada wa dola milioni 10 iliyopatiwa na Australia na kuzitaka nchi za Kiarabu na Kiislamu zikate uhusiano wao na nchi hiyo kutokana na uamuzi wake wa kuitambua Quds kama mji mkuu wa utawala haramu wa Israel.
-
Palestina inahitaji dola milioni 350 za misaada ya kibinadamu: OCHA
Dec 18, 2018 03:25Wapalestina ambao ardhi zao zinakaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Isarel wanahitaji msaada wa dola milioni 350 mwaka 2019 kwa ajili ya huduma za kimsingi kama chakula, ulinzi, huduma za afya, malazi, maji na usafi.
-
PLO yawataka Wapalestina kupambana na wanajeshi wa Israel
Dec 14, 2018 00:53Chama cha Ukombozi wa Palestina PLO kimewataka wananchi wa Palestina kutokubali kudhalilishwa na wasimame imara kupambana na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hamas yalipiza kisasi baada ya wanachama wake 2 kuuawa na jeshi la Israel
Dec 13, 2018 10:24Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imewaangamiza Wazayuni wawili kwa kuwafyatulia risasi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, chini ya masaa 24 baada ya jeshi katili la Israel kuwaua shahidi Wapalestina watatu, wakiwamo wanachama wawili wa harakati hiyo ya Muqawama.
-
Mshauri wa zamani: Saudia iliidhinisha mauaji ya Yassir Arafat
Dec 11, 2018 03:18Aliyekuwa mshauri mwandamizi wa Yasser Arafat, Rais wa zamani wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amefichua kuwa kiongozi huyo wa zamani wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) hakufa kifo cha kawaida baada kuugua, bali aliuawa, na kwamba Saudi Arabia ndiyo iliyoidhinisha mauaji yake.
-
Pigo la kihistoria kwa Marekani katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, katika mwaka wa kwanza wa uamuzi wa Trump dhidi ya Quds
Dec 07, 2018 20:52Muswada uliokuwa umependekezwa na Marekani dhidi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS katika Baraza la Kuu la Umoja wa Mataifa haukupasishwa na kumfanya Nikki Haley, balozi na mwakilishi wa kudumu wa Marekani katika Umoja wa Mataifa ashuhudie pigo la kihistoria dhidi ya nchi yake katika siku zake hizi za mwisho za majukumu yake katika umoja huo.
-
Makundi ya Muqawama Palestina: Marekani, Israel zimepata pigo kubwa UN
Dec 07, 2018 11:07Makundi ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina ya Hamas na Jihadu Islami yamesema kupigwa mweleka katika Baraza la Kuu la Umoja wa Mataifa muswada wa kuilaani Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) na kuitaja kama kundi la kigaidi ni pigo kubwa kwa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Umuhimu wa mkutano wa Ofisi za Kieneo za Kuususia Utawala wa Kizayuni
Dec 06, 2018 02:39Mkutano wa 92 wa Ofisi za Kieneo za Kuususia Utawala wa Kizayuni umefanyika katika makao makuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu mjini Cairo Misri na kushirikishwa wawakilishi kutoka nchi za Kiarabu na wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu, OIC.
-
Hamas yaiomba Afrika Kusini kusadia mapambano ya ukombozi ya Wapalestina
Dec 04, 2018 11:15Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imeiomba Afrika Kusini izidishe uungaji mkono na misaada yake kwa taifa la Palestina katika mapambano yake ya ukombozi dhidi ya utawala haramu wa Israel.