-
Bendera za Israel, US zachomwa moto Brazil katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina
Jul 02, 2024 06:12Wananchi wenye hasira wa Brazil wamechoma moto bendera za Israel, Marekani na Umoja wa Ulaya wakati wa maandamano ya kuunga mkono Palestina na kupinga mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza.
-
Sayyid Nasrullah: Kukombolewa Palestina ndio ushindi wa mwisho
Jun 30, 2024 02:14Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, ushindi wa mwisho ni kukombolewa Palestina na kuondolewa eneo la Asia Magharibi kutoka katika udhibiti utawala wa Marekani.
-
Erdogan: Nchi za Magharibi zimekuwa mateka wa mtu kichaa kama Netanyahu
Jun 27, 2024 02:58Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan alisema jana Jumatano kwamba nchi yake inasimama bega kwa bega na Lebanon kutokana na mvutano unaozidi kuongezeka na utawala wa Kizayuni wa Israel, na amezitaka pande za kikanda kumuunga mkono katika msimamo huo.
-
CAIR: Dunia ina wajibu wa kukomesha mauaji ya watoto Gaza
Jun 26, 2024 02:18Kundi la kutetea haki za Waislamu na kiraia nchini Marekani limeeleza kusitikishwa na hali mbaya ya watoto katika Ukanda wa Gaza, na kusisitiza kuwa jamii ya kimataifa na wajibu wa kusimamisha mauaji ya watoto Gaza.
-
Njaa yaenea Gaza kutokana na kuendelea mashambulizi ya utawala wa Kizayuni
Jun 25, 2024 07:44Mkuu wa Ofisi ya Habari ya Serikali ya Palestina katika Ukanda wa Gaza amesisitiza kuwa njaa inazidi kuongezeka katika keneo kila siku kufuatia kushtadi mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya wakazi wa ukanda huo.
-
Borrell: Hali ya mambo ya Gaza haielezeki kufuatia mashambulizi ya Israel
Jun 24, 2024 11:19Josep Borrel Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa hali ya mambo katika Ukanda wa Gaza ambako Israel inaendeleza mashambulizi yake ya mauaji ya unati tangu Oktoba mwaka jana haielezeki.
-
HAMAS: Kuendelea kutambuliwa Palestina kutahitimisha unazi wa Kizayuni
Jun 22, 2024 11:19Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS sanjari na kukaribisha kwa mikono miwili na kupongeza hatua ya Armenia ya kulitambua rasmi taifa huru la Palestina, imesisitiza kuwa mwenendo huo wa mataifa ya dunia kuitambua Palestina kama nchi huru utapelekea kufikia ukingoni unazi wa Kizayuni.
-
Bagheri Kani: Mataifa ya eneo yachukue hatua za kukomesha mauaji ya kimbari Gaza
Jun 20, 2024 12:48Kaimu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, hali ya eneo na maslahi ya mataifa ya eneo hili yanahitaji kutumia uwezo wao wote kusimamisha mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Ghaza na kuwaunga mkono wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
-
Umoja wa Mataifa: Vita vimeigeuza Gaza kuwa Jahanamu ya duniani
Jun 18, 2024 02:43Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, vita vimeligeuza eneo la Ukanda wa Gaza kuwa Jahanamu ya duniani.
-
Jeshi la Yemen: Meli mbili zinazozama ni zawadi yetu ya Idi kwa muqawama wa Palestina
Jun 17, 2024 03:19Msemaji wa jeshi la Yemen ametangaza kuwa, meli mbili zinazozama ni zawadi ya Eid al-Adh'haa ya jeshi la Yemen kwa muqawama wa Palestina kutokana na kusimama kwao kidete.