-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran asisitiza kusitishwa haraka jinai za utawala wa Kizayuni; azungumza na Hania na Al Nakhaleh
Oct 23, 2023 09:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezungumza kwa simu kwa nyakati tofauti na viongozi wa muqawama wa Palestina na kusisitiza kusitishwa haraka iwezekanavyo jinai za utawala wa Kizayuni za mauaji dhidi ya raia wa Palestina.
-
Idadi ya mashahidi wa Gaza Palestina yafikia 5087
Oct 23, 2023 08:40Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa, zaidi ya Wapalestina 5,000 wameuawa shahidi na wengine zaidi ya 15,000 kujeruhiwa kutokana na hujuma na mashambulio ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Viongozi wa nchi za Kiarabu walaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, wahimiza juhudi mpya za amani Palestina
Oct 21, 2023 23:50Viongozi wa nchi za Kiarabu wametoa wito wa kuanzishwa upya juhudi za amani kati ya Israel na Palestina ili kukomesha uvamizi wa Israel na kutatua mzozo unoendelea kwa miongo kadhaa kati ya pande hizo mbili, huku utawala haramu Israel ukiendeleza mashambulizi ya kikatili dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza.
-
Mkutano wa amani wa kutatua mzozo wa Hamas na utawala wa Kizayuni wa Israel unafanyika Cairo
Oct 21, 2023 10:54Mkutano wa kimataifa wa amani umeanza leo asubuhi mjini Cairo, Misri, ambapo viongozi wa kiserikali kutoka mataifa mbalimbali pamoja na taasisi za kimataifa walianza kujadili maendeleo na mustakabali wa mzozo wa utawala wa Kizayuni wa Israel na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS.
-
Zakzaky: Mauaji ya halaiki ya Gaza yanaonesha udhaifu wa Israel
Oct 19, 2023 23:28Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria amesema mauaji makubwa ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza yameonyesha kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel una udhaifu mkubwa.
-
Jumuiya ya OANA yataka kulindwa waandishi wa habari Gaza
Oct 19, 2023 23:28Jumuiya ya Mashirika ya Habari ya Asia-Pasifiki (OANA) imesisitizia haja ya kudhaminiwa usalama na ulinzi waandishi wa habari walioko katika Ukanda wa Gaza.
-
Raisi: Veto ya US katika Baraza la Usalama ni 'dhulma maradufu' kwa Wapalestina
Oct 19, 2023 11:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hatua ya Marekani ya kulipigia kura ya turufu azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linalotaka kusimamishwa mashambulizi na jinai za Israel dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza ni dhulma maradufu dhidi ya Wapalestina na ubinadamu.
-
Iran na Tunisia zafanya mazungumzo ya namna ya kuwasaidia wananchi wa Ghaza
Oct 19, 2023 02:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo na waziri mwenzake wa mambo ya nje wa Tunisia mjini Jeddah, Saudi Arabia na pande mbili zimejadiliana njia za kuwasaidia wananchi wa Ghaza na kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Shirika: Israel inaua watoto 100 wa Kipalestina kila siku
Oct 18, 2023 08:55Shirika moja la kutetea haki za binadamu lenye makao yake mjini Geneva Uswisi limesema kwa wastani utawala haramu wa Israel unaua shahidi watoto 100 wa Kipalestina katika kila saa 24 katika Ukanda wa Gaza.
-
HAMAS: Tutawaachia Waisraeli mkabala wa kuachiwa huru wafungwa 6,000 wa Kipalestina
Oct 18, 2023 00:21Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imesema iko tayari kuwaachia huru mateka wa Kizayuni iliowakamata katika Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa, mkabala wa utawala haramu wa Israel kuwaachia huru maelfu ya wafungwa wa Kipalestina.