-
Russia: BRICS kuanzisha mfumo wa malipo wa 'dijitali' kwa wanachama
Mar 28, 2025 23:42Waziri wa Fedha wa Russia amesema kuwa nchi wanachama wa kundi la BRICS zinachunguza hatua kadhaa za ubunifu wa kifedha ikiwemo kuanzisha mfumo wa malipo wa kidijitali ili kutoa huduma za kifedha ndani ya kambi hiyo ya kiuchumi.
-
Marekani na Ulaya zashindwa kukabiliana na changamoto za kimataifa
Mar 28, 2025 02:34Mark Rutte, Katibu Mkuu wa NATO amesisitiza juu ya umoja wa pande mbili za Bahari ya Atlantiki na kusema kuwa changamoto za kiusalama duniani ni kubwa kiasi kwamba Ulaya na Marekani pake yazo haziwezi kukabiliana nazo.
-
Rais Putin: Watu wa Magharibi hawaielewi Russia
Mar 27, 2025 22:57Rais Vladimir Putin amesema baadhi ya watu katika nchi za Magharibi hawaielewi Russia, lakini amesisitiza kuwa ukweli huo hauwezi kutatiza hata kidogo ustawi na maendeleo ya nchi hiyo.
-
Upinzani wa serikali ya Trump dhidi ya hatua za Ulaya za kupinga Russia
Mar 25, 2025 23:09Baada ya kuchaguliwa tena kwa mara ya pili Rais Donald Trump wa Marekani sasa amegeukia mazungumzo ya moja kwa moja na Russia nchini Saudi Arabia ili kutimiza ahadi aliyotoa ya kuhitimisha vita huko Ukraine ambapo jumbe za Marekani na Russia tayari zimefanya duru ya pili ya mazungumzo huko Riyadh Saudi Arabia kuhusiana na suala hilo.
-
Mapatano mapya ya nchi za Umoja wa Ulaya dhidi ya Russia
Mar 24, 2025 07:04Kwa kutilia maanani jaribio la utawala wa Trump la kuanzisha usitishaji vita nchini Ukraine kwa kuilazimisha ikubali masharti yaliyowekwa na Russia na upinzani wa nchi za Umoja wa Ulaya dhidi ya suala hili, na kwa upande mwingine madai ya baadhi ya viongozi wa Ulaya kuhusu vitisho vya Russia dhidi ya bara hilo, nchi hizo sasa zimechukua hatua mpya kwa ajili ya kukabiliana na Moscow.
-
Balozi wa Trump: Russia haitaki kushambulia Ulaya
Mar 22, 2025 23:10Mjumbe maalum wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati (Asia Magharibi), Steve Witkoff amepuuzilia mbali madai kwamba Russia ina nia ya kuzivamia nchi nyingine za Ulaya, akisisitiza kuwa hofu hizo ni za "kipuuzi".
-
Wanachama wa EU wakubaliana kuongeza nguvu za kijeshi mkabala wa Russia
Mar 22, 2025 01:03Waziri Mkuu wa Poland amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zimekubaliana hadi kufikia mwaka 2030 kuongeza uwezo wao wa kijeshi ili kuweza kukabiliana na mshambulizi yoyote ya Russia.
-
Niger yajitoa rasmi katika Jumuiya ya Nchi Zinazozungumza Kifaransa, Francophone
Mar 19, 2025 00:44Niger imejiondoa rasmi katika Jumuiya ya Kimataifa ya nchi zinazozungumza Kifaransa (OIF) au Francophone sambamba na juhudi zinazoendelea kufanywa na taifa hilo la Afrika Magharibi za kuvunja uhusiano na kujitenga na mkoloni wake wa zamani, Ufaransa.
-
Zakharova: Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani bado anakabiliwa na vikwazo vya Russia
Mar 16, 2025 22:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema kuwa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, hajaondolewa kwenye orodha ya vikwazo ya Russia, na kila kinachosemwa kuhusu suala hili ni uongo.
-
Russia yataka kuhuishwa makubaliano ya JCPOA
Mar 13, 2025 23:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergei Lavrov amesisitiza uungaji mkono wa Moscow kwa kufufuliwa mkataba wa kihistoria uliotiwa saini na Iran na mataifa mengine sita yenye nguvu duniani mwaka 2015.