-
Russia yakosoa juhudi za Magharibi za kurefusha vita vya Ukraine
Apr 21, 2022 04:41Waziri wa Ulinzi wa Russia, Sergei Shoigu amesema kwamba Marekani na nchi nyingine za Magharibi zimefanya jitihada kubwa za kurefusha muda wa operesheni ya kijeshi ya Russia nchini Ukraine.
-
Kukosolewa unafiki wa Marekani kuhusu suala la haki za binadamu
Apr 20, 2022 22:20Ilhan Omar, mbunge wa Kiislamu katika Congress ya Marekani amesema kuwa madai yanayotolewa na utawala wa Wadhington kuhusu haki za binadamu duniani ni ya kinafiki, na kusisitiza kuwa kama nchi hiyo inataka kuishtaka Russia katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kuhusiana na tuhuma zinazotolewa dhidi yake kuhusu vita vya Ukraine, inapasa kwanza yenyewe ijiunge na kuwa mwanachama wa mahakama hiyo.
-
Russia yawapatia wanajeshi wa Ukraine makataa mapya ili kujisalimisha huko Mariupol
Apr 20, 2022 22:19Russia imewapatia makaa mapya wanajeshi wa Ukraine ambao bado wapo katika mji wa kistratejia wa bandari wa Mariupol huko Kusini mwa Ukraine; huku Moscow ikiendeleza mashambulizi yake upande wa Mashariki mwa nchi hiyo.
-
Russia yatahadharisha juu ya uwezekano wa kupigana na Nato
Apr 17, 2022 21:59Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetahadharisha juu ya uwezekano wa kujiri mapigano ya muda mrefu baina ya nchi hiyo na Shirika Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) katika katika eneo la Ncha ya Kaskazini.
-
Russia yaonya itaweka silaha za nyuklia Baltic iwapo Sweden na Finland zitajiunga na NATO
Apr 16, 2022 21:50Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Russia ameonya kuwa, iwapo Finland na Sweden zitajiunga na muungano wa kijeshi wa NATO, basi Russia itazitambua nchi hizo mbili kuwa maadui.
-
Russia yaishutumuu Israel kwa kuigeuza Ghaza kuwa jela kubwa ya wazi duniani
Apr 16, 2022 02:48Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imeushutumu utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuligeuza eneo la Ghaza huko Palestina kuwa jela kubwa ya wazi duniani.
-
Russia: Hakuna Mwafrika anayepigana kwa niaba ya Moscow nchini Ukraine
Apr 14, 2022 23:33Balozi wa Russia nchini Kenya amekadhibisha madai kuwa Moscow imekodisha mamluki wa Kiafrika kwenda kupigana kwa niaba yake nchini Ukraine.
-
Mfumko wa bei za bidhaa Marekani umesababishwa na vikwazo dhidi ya Russia
Apr 14, 2022 23:30Gazeti la Washington Post limeripoti kuwa, vikwazo vya Washington dhidi ya Russia vimekuwa chachu ya kushadidisha mfumko wa bei za bidhaa unaoshuhudiwa nchini Marekani.
-
Lavrov: Lengo la operesheni maalumu ya Russia nchini Ukraine ni kukomesha udhibiti wa Marekani duniani
Apr 12, 2022 03:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema lengo la operesheni maalumu ya Moscow nchini Ukraine ni kukomesha udhibiti wa Marekani duniani.
-
Khatibzadeh: Marekani bado haijaonyesha nia ya kufikia makubaliano
Apr 11, 2022 03:48Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema kuwa, Marekani bado haijaonyesha nia ya kutosha ya kufikia makubaliano katika mazungumzo ya nyuklia yanayoendelea huko Vienna nchini Austria na kuongeza kuwa: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haiathiriwi na kampeni za vyombo vya habari na matamshi yanayokinzana.