-
UN yataka kuachiwa huru wanaharakati wanawake walioko jela Saudi Arabia
Jul 09, 2020 22:37Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limezitaka nchi nyingine duniani kuiwekea Saudi Arabia mashinikizo ili kuwaachia huru wanaharakati wa kijamii wanawake waliofungwa jela nchini humo.
-
Uturuki: Saudia haina ustahiki wa kuendesha kesi ya wauaji wa Khashoggi
Jul 06, 2020 06:48Mshauri wa Rais wa Uturuki amesisitiza kuwa, Saudi Arabia haina ustahiki wa kuendesha kesi za wauaji wa Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari raia wa Saudia aliyeuliwa kinyama ndani ya ubalozi mdogo wa nchi hiyo mjini Istanbul, Uturuki.
-
Gazeti la Kisaudi lililomvunjia heshima Ayatullah Sistani lalazimika kubadilisha msimamo
Jul 04, 2020 23:36Malalamiko makubwa na upinzani mkali wa viongozi na mirengo tofauti ya kisiasa ya Iraq, sambamba na hatua nyingi zilizochukuliwa na wananchi na makundi ya muqawama wa Kiislamu katika mitandao ya kijamii dhidi ya hatua ya gazeti la Kisaudi la Ash-Sharqul-Awsat ya kuchora katuni ya kumvunjia heshima kiongozi wa juu wa kidini wa nchini Iraq, hatimaye zimepelekea gazeti hilo lilazimike kuondoa katuni hiyo.
-
Kamisheni ya UNESCO ya Yemen yataka Saudia ishtakiwe ICC
Jun 23, 2020 23:18Kamisheni ya Kitaifa ya Yemen katika Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) imeutaka Umoja wa Mataifa uangalie upya uamuzi wake wa kufuta jina la Saudi Arabia na washirika wake katika vita vya Yemen kwenye orodha nyeusi ya nchi zinazoua watoto na kuvunja haki zao, na badala yake uwasilishe faili la jinai hizo katika Mahakama ya Kimataifa ya Jina (ICC).
-
Jeshi la Yemen latekeleza oparesheni ya kujihami ndani ya ardhi ya Saudia
Jun 23, 2020 06:16Msemaji wa Majeshi ya Yemen amesema majeshi ya nchi hiyo yametekeleza oparesheni maalumu ndani kabisa ya ardhi ya Saudi Arabia.
-
Deni la Saudia laongezeka kwa asilimia 375 wakati wa Bin Salman
Jun 22, 2020 03:00Data za Benki ya Dunia zinaonesha kuwa deni la nje la Saudi Arabia limepanda vibaya mno tangu Mohammad bin Salman alipopewa cheo cha kurithi kiti cha ufalme wa nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa; mateka wa siasa za pesa na mabavu za Saudi Arabia na Marekani
Jun 19, 2020 03:40Mtazamo wa kindumakuwili wa Umoja wa Mataifa Kuhusu vita vya Yemen na suala la kushambuliwa shirika la mafuta la Aramco la Saudi Arabia, unaonyesha kuwa taasisi hiyo ya kimataifa ambayo imepewa jukumu la kulinda amani na usalama duniani imesahau jukumu lake hilo.
-
Ripoti ya UN: Wayemeni zaidi ya milioni 20 wanakabiliwa na hatari ya kupatwa na corona
Jun 05, 2020 03:22Shirika la Programu na Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) limetangaza kuwa, zaidi ya Wayemeni milioni 20 wanasumbuliwa na njaa ya muda mrefu na wamo katika hatari ya kupatwa na virusi vya corona.
-
Hali ya kiafya ya kiongozi wa HAMAS anayeshikiliwa katika jela ya Saudia yazidi kuzorota
May 29, 2020 06:07Hali ya kiafya ya Muhammad Khidhri, mwakilishi wa harakati ya muqawama wa Kiislamu wa Palestina HAMAS ambaye alitiwa mbaroni miezi kadhaa iliyopita nchini Saudia, imezidi kuwa mbaya.
-
Wakati Saudia na Imarati zinapoitumia vibaya Sudan na baadaye kuiacha "solemba"
May 26, 2020 02:19Kwa muda sasa Sudan imebadilisha misimamo yake ya kisiasa kama njia ya kuvutia misaada ya kifedha kutoka kwa nchi kama Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Saudi Arabia lakini nchi hizo hazioneshi utashi wowote wa kuitatulia Khartoum matatizo yake zaidi ya kuitumia tu kufanikishia malengo yao binafsi.