-
Safari ya Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani nchini Saudia
Apr 30, 2018 22:15Katika safari yake ya kwanza kwa ajili ya kukutana na viongozi wa nchi washirika wa Washington, Mike Pompeo, Waziri Mpya wa Mambo ya Nje wa Marekani ametembelea Riyadh, mji mkuu wa Saudia.
-
Saudia: Tunaunga mkono kuwekewa vikwazo zaidi Iran
Apr 29, 2018 22:11Adel al Jubeir, waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia amesema kuwa Riyadh inaunga mkono kuwekewa vikwazo zaidi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Jeshi la Yemen: Saudia iondoe watu kwenye ofisi za serikali na viwanda, tutalipa kisadi damu ya al-Sammad
Apr 25, 2018 09:58Kamandi kuu ya jeshi la Yemen imetoa taarifa kufuatia kuuawa shahidi na muungano vamizi wa Saudia Saleh al-Sammad, Kiongozi wa Baraza Kuu la Kisiasa la nchi hiyo, na kusema Saudia inatakiwa kuhamisha watu haraka kutoka kwenye viituo vyote vya serikali, wizara na viwanda.
-
Kiongozi wa Baraza la Kisiasa Yemen auawa katika hujuma ya Saudia
Apr 23, 2018 12:33Kiongozi wa Baraza Kuu la Kisiasa Yemen, Saleh Saleh al-Sammad ameuawa katika hujuma ya ndege za kivita za Saudia Arabia katika mkoa wa al-Hudydah.
-
Utawala wa Aal Saud wawapiga marufuku mahujaji kuzuru "Pango la Hira"
Apr 22, 2018 03:37Wizara ya Hija na Umra ya Saudi Arabia imepiga marufuku mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Allah kuzuru maeneo ya Mlima Nuru na Pango la Hira.
-
Habari za kutatanisha zagubika tukio la milio ya risasi iliyosikika karibu na kasri la Mfalme wa Saudia
Apr 22, 2018 03:29Baada ya kimya cha saa kadhaa cha maafisa na vyombo vya habari vya Saudi Arabia kuhusu milio mingi ya risasi iliyosikika jana usiku katika mji mkuu Riyadh, shirika rasmi la habari la nchi hiyo limedai kuwa ufyatuaji huo wa risasi uliotokea ulisababishwa na droni ndogo bandia iliyokuwa ikipaa karibu na kasri la mfalme wa nchi hiyo.
-
Maafisa wanne wa jeshi la Saudia waangamizwa katika mkoa wa 'Asir
Apr 19, 2018 23:43Maafisa wanne wa jeshi la Saudi Arabia wameangamizwa katika shambulio la ufyatuaji risasi lililotokea kwenye kituo kimoja cha upekuzi mkoani 'Asir kusini magharibi mwa nchi hiyo.
-
Saudi Arabia yaendelea kuishambulia Yemen kwa mabomu yaliyopigwa marufuku
Apr 19, 2018 09:21Saudi Arabia imeendelea na hujuma zake za kijeshi huko Yemen na kuendelea kutumia mabomu yaliyopigwa marufuku kimataifa.
-
Wanawake wahajiri wa Kiafrika wanadhalilishwa kingono katika jela zinazosimamiwa na Saudia na UAE, Aden
Apr 19, 2018 03:21Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR yameripoti kuwa wanawake wahajiri wa Kiafrika wanakashifiwa na kudhalilishwa kingono katika mji wa Aden kusini mwa Yemen ambao unadhibitiwa na vikosi vya Imarati (UAE) na Saudi Arabia.
-
HRW: Mamluki wa Imarati wanawabaka wahajiri wa Kiafrika Yemen
Apr 18, 2018 03:08Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema mamluki wanaofadhiliwa na kuungwa mkono na Umoja wa Falme za Kiarabu nchini Yemen wanawabaka na kuwalawiti wahajiri wa kike na kiume raia wa Afrika katika nchi hiyo masikini ya Kiarabu.