-
Mapigano makali yaripotiwa kandokando ya ikulu ya rais mjini Khartoum, Sudan
Mar 02, 2025 03:45Baadhi ya vyanzo vya ndani vimeripoti kuwa Jeshi la Sudan limefanya mashambulizi makali dhidi ya ngome za wapiganaji wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) mjini Khartoum na kwamba mapigano makali yanashuhudiwa karibu na ikulu ya rais.
-
WFP yasimamisha usambazaji wa chakula Darfur Kaskazini, Sudan
Mar 01, 2025 03:44Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesitisha usambazaji wa chakula cha msaada katika kambi ya wakimbizi ya Zamzam nchini Sudan kutokana na kushtadi mapigano kati ya jeshi la serikali na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF).
-
Mkuu wa haki za binadamu wa UN atadhaharisha juu ya hali mbaya ya mgogoro nchini Sudan
Feb 28, 2025 04:02Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi aligusia mzozo unaozidi kuongezeka nchini Sudan na kutoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka za kimataifa ili kuzuia ukatili zaidi, njaa na watu wengi kuhama makazi yao.
-
Karibu wagonjwa 1,200 zaidi wa kipindupindu wameripotiwa katika jimbo la White Nile, Sudan
Feb 23, 2025 04:10Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa kesi 1,197 za ugonjwa wa kipindupindu, vikiwemo vifo 83 vilivyosababishwa na ugonjwa huo vimesajiliwa katika jimbo la White Nile siku mbili zilizopita.
-
Pezeshkian: Iran inakaribisha kuhuishwa uhusiano wake na Sudan
Feb 19, 2025 08:41Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema Jamhuri ya Kiislamu inakaribisha kwa mikono miwili kurejeshwa kwa uhusiano wa nchi hii na Sudan, akisisitiza kuwa nchi za Kiislamu zinapaswa kuepuka mivutano na kukata uhusiano baina yao.
-
Sudan kukabiliana na watakaojaribu kuunda serikali nyingine
Feb 19, 2025 08:39Mjumbe wa Baraza Kuu la Sudan amesema serikali ya nchi hiyo "itapambana na yeyote anayetaka kuanzisha serikali nyingine" katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Spika Ghalibaf: Iran inaunga mkono uthabiti nchini Sudan
Feb 18, 2025 04:08Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Mohammad Baqer Ghalibaf amesema Jamhuri ya Kiislamu inaunga mkono juhudi za kurejeshwa utulivu na uthabiti nchini Sudan, sanjari na kuundwa "utawala wa umoja" ambao utahakikisha kuwa taifa hilo lina mamlaka kamili ya kujitawala.
-
Sudan yaafiki kuanzishwa nchini humo kambi ya jeshi la wanamaji la Russia
Feb 12, 2025 23:22Khartoum na Moscow zimekubaliana juu ya kuanzishwa kituo cha jeshi la wanamaji la Russia nchini Sudan.
-
IOM: Vita vya Sudan vimeongeza idadi ya wakimbizi wa ndani Pembe ya Afrika
Feb 04, 2025 23:10Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema idadi ya wakimbizi wa ndani (IDP) katika Pembe ya Afrika iliongezeka hadi milioni 20.75 kufikia mwishoni mwa mwaka uliopita wa 2024.
-
Watu 44 wauawa katika shambulio la waasi wa SPLM-N huko Kordofan Kusini
Feb 04, 2025 03:59Maafisa wa Sudan wametangaza kuwa watu wasiopungua 44 wameuawa na 28 kujeruhiwa katika shambulio lililotekelezwa na waasi wa harakati ya SPLM-N inayoongozwa na Abdelaziz al Hilu katika makao makuu ya jimbo la Korofan Kusini kusini mwa Sudan.