-
Kutiwa saini makubaliano ya amani nchini Sudan na mustakbali wa kisiasa wa nchi hiyo
Aug 06, 2019 03:43Hatimaye baada ya mgogoro wa kisiasa, machafuko na maandamano ya miezi kadhaa, wanajeshi wa Sudan na viongozi wa vyama vya upinzani wametila saini tamko la katiba litakalowaongoza katika kuunda serikali ya mpito.
-
Independent: Wanawake wamepuuzwa katika mfumo mpya wa utawala Sudan
Aug 05, 2019 07:42Gazeti la Independent linalochapishwa nchini Uingereza limendika kuwa, mfumo mpya wa utawala nchini Sudan umepuuza nafasi na mchango mkubwa wa wanawake katika mapinduzi yaliyouondoa madarakani utawala wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Omar al Bashir.
-
Wanajeshi na wapinzani Sudan watiliana saini tamko la kuunda serikali ya mpito
Aug 05, 2019 03:52Hatimaye baada ya vuta nikuvute wanajeshi na viongozi wa waandamanaji nchini Sudan wametiliana saini tamko la katiba litakalowaongoza katika kuunda serikali ya mpito.
-
Maafikiano ya kuunda serikali ya mpito nchini Sudan
Aug 03, 2019 07:15Baada ya kupita miezi kadhaa ya mzozo wa kisiasa nchini Sudan hatimaye Baraza la Kijeshi la Mpito na muungano mkuu wa wapinzani wa nchi hiyo wameafikiana juu ya tamko la katiba ambalo litapelekea kubuniwa serikali ya mpito nchini humo.
-
Wasudan wafikia mapatano juu ya tangazo la katiba ya kipindi cha mpito
Aug 03, 2019 02:50Baraza la Kijeshi linalotawala Sudan na vyama vya upinzani wamefikia makubaliano juu ya tangazo la katiba ambayo itapelekea kuundwa serikali ya kipindi cha mpito nchini humo.
-
Baraza la kijeshi Sudan lawaweka kizuizini askari tisa baada ya mauaji ya El-Obeid
Aug 02, 2019 10:13Msemaji wa baraza la kijeshi nchini Sudan amesema, askari tisa wa Vikosi vya Msukumo wa Haraka (RSF) wameachishwa kazi na kuwekwa kizuizini kuhusina na machafuko yaliyotokea hivi karibuni katika miji ya Omdurman na El-Obeid.
-
Waandamanaji wanne wauawa katika mji wa Omdurman nchini Sudan
Aug 02, 2019 03:33Waandamanaji wanne wanaripotiwa kuuawa kwa kupigwa risasi katika maandamano yaliyofanyika jana katika mji wa Omdurman huko nchini Sudan, huku makumi ya wengine wakijeruhiwa.
-
Watawala wa kijeshi Sudan na upinzani kuendelea na mazungumzo kuhusu uongozi wa mpito
Aug 01, 2019 11:15Wawakilishi wa baraza la kijeshi linalotawala Sudan na wa muungano mkuu wa upinzani wamepiga hatua katika masuala yenye mvutano kwenye mazungumzo ya kipindi cha mpito kutoka utawala wa kijeshi kuelekea wa kiraia na wanatazamiwa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana katika muda wa saa 24 zijazo.
-
Umoja wa Afrika wataka wauaji wa wanafunzi wa Sudan wafikishwe mahakamani
Aug 01, 2019 02:54Umoja wa Afrika (AU) umeitaka serikali ya Sudan kuwafikisha mahakamani askari waliohusika na mauaji ya wanafunzi 6 waliokuwa wakiandamana kulalamikia hali mbaya ya maisha.
-
Wasudan watolewa mwito wa kufanya "maandamano ya mamilioni" leo
Jul 31, 2019 22:28Jumuiya ya ajira nchini Sudan imetoa mwito wa kufanyika "maandamano ya mamilioni" nchini kote hii leo.