-
Viongozi watatu wa upinzani nchini Sudan watiwa mbaroni baada ya kukutana na Abiy Ahmed
Jun 08, 2019 23:01Jeshi la Sudan limewatia mbaroni viongozi watatu wa upinzani muda mfupi baada ya viongozi hao kukutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed.
-
Wapinzani Sudan wakubali kwa masharti Ethiopia kuwa mpatanishi
Jun 08, 2019 02:12Muungano wa upinzani nchini Sudan umeafiki kuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed awe mpatanishi baina yao na Baraza la Mpito la Kijeshi ili kutatua mgogoro mkubwa wa kisiasa unaotokota nchini humo.
-
Middle East Eye: Shambulizi dhidi ya waandamanaji Sudan limefanyika kwa ruhusa ya Saudia
Jun 07, 2019 21:48Mtaalamu wa masuala ya kijeshi wa Sudan amekiambia kituo cha habari cha Middle East Eye cha Uingereza kwamba, Kiongozi wa Baraza la Kijeshi la Mpito huko Sudan Jenerali Abdel Fattah al Burhan aliidhinishwa na Saudi Arabia na waitifaki wake kufanya mashambulizi dhidi ya raia waliokuwa wamekusanyika na kufanya mgomo mbele ya makao makuu ya jeshi la nchi hiyo Jumatatu iliyopita ambalo liliua zaidi ya raia mia moja.
-
Kuongezeka mgogoro wa Sudan na mustkabali usiojulikana wa nchi hiyo
Jun 07, 2019 08:01Kufuatia kuongezeka mgogoro wa Sudan ambao umepelekea mamia ya wapinzani kuuawa na kujeruhiwa, Umoja wa Afrika umesimamisha kwa muda uanachama wa nchi hiyo hadi pale raia watakapokabidhiwa madaraka.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia aelekea Sudan kupatanisha jeshi na raia
Jun 07, 2019 02:47Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed leo anatazamiwa kuitembelea Sudan kwa lengo la kujaribu kuwapatanisha watawala wa kijeshi na makundi ya raia kufuatia kuendelea mgoggoro nchini humo baada ya Omar al Bashir kuondolewa madarakani.
-
Umoja wa Mataifa: Tunaondoa askari wetu wa kusimamia amani nchini Sudan
Jun 06, 2019 22:37Kufuatia kuzorota hali ya usalama nchini Sudan, Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba utaondoa maafisa wake wasio wa kijeshi waliokuwa wakisimamia amani nchini humo.
-
Umoja wa Afrika wasimamisha uanachama wa Sudan katika jumuiya hiyo
Jun 06, 2019 07:47Umoja wa Afrika AU umechukua uamuzi wa kusimamisha uanachama wa Sudan katika jumuiya hiyo kubwa zaidi barani Afrika mpaka pale Baraza la Kijeshi litakapokabidhi madaraka ya nchi kwa utawala wa kiraia.
-
Waandamanaji waliouawa na maafisa usalama Sudan wapindukia 108
Jun 06, 2019 02:07Idadi ya watu waliouawa katika wimbi jipya la ukatili na utumiaji wa nguvu kupita kisiasa wa maafisa usalama wa Sudan dhidi ya waandamanaji wanaotaka kukabidhiwa madaraka kwa utawala wa kiraia imepindukia watu 100.
-
Wapinzani Sudan wazitaka Saudia, Misri na Imarati ziache kuingilia mambo ya ndani ya nchi yao
Jun 05, 2019 07:29Wapinzani wa utawala wa kijeshi nchini Sudan wamezitaka badhi ya nchi za Saudi Arabia, Imarati na Misri ziache kuingilia mambo ya ndani ya nchi hiyo.
-
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lafanya kikao cha dharura kujadili mgogoro wa Sudan
Jun 05, 2019 03:37Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya kikao cha dharura na kisicho cha wazi kujadili hali ya mambo nchini Sudan.