-
Waziri wa Ulinzi wa Iran avipongeza vikosi vilivyokabiliana na magaidi wa Daesh nchini Syria
Sep 05, 2018 22:29Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, vikosi vya kijeshi vilivyopambana na magaidi nchini Syria vimeweza kusambaratisha njama kubwa iliyokuwa imeratibiwa dhidi ya usalama wa Mashariki ya Kati.
-
Waziri wa Syria: Kuna baadhi ya nchi zinafanya njama kufelisha maridhiano Idlib
Sep 04, 2018 22:01Waziri wa Maridhiano ya Kitaifa nchini Syria amesema kuwa, kuna baadhi ya nchi zinafanya njama ya kufelisha mpango wa usuluhishi katika mkoa wa Idlib, kaskazini magharibi mwa Syria.
-
Hizbullah: Marekani haina ubavu wa kuwawekea masharti walioshinda vita Syria
Sep 04, 2018 03:37Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imesema kuwa Marekani ambayo sera zake za kuyasaidia makundi ya kigaidi kwa ajili ya kuindoa madarakani serikali halali ya Syria zimefeli na kushindwa haina haki na ubavu wa kutoa masharti ya kuondoka washauri wa kijeshi wa Iran na wapiganaji wa Hizbullah nchini Syria ambao wameshinda vita dhidi ya magaidi.
-
Ufaransa yakiri, Syria imeshinda vita vya ndani
Sep 03, 2018 03:09Ufaransa na Uingereza ambazo ni nchi mbili wanachama katika Umoja wa Ulaya (EU) tangu mwaka 2011 zikiwa katika muungano wa nchi za Magharibi na za Kiarabu wa kutaka kuiondoa madarakani serikali halali ya Syria, zimekuwa zikitoa misaada ya pande zote kwa makundi ya waasi na ya kigaidi kwa shabaha eti ya kuipindua serikali ya Rais Bashar Assad.
-
Maneva makubwa ya kijeshi ya Russia Bahari ya Mediterranean, majibu kwa vitisho vinavyozidi kuongezeka vya Marekani dhidi ya Syria
Sep 02, 2018 01:26Ushindi mkubwa linaoendelea kuupata jeshi la Syria na waitifaki wake katika maeneo tofauti ya nchi hiyo, na hatua ya jeshi hilo ya kujiandaa hivi sasa kuusafisha mkoa wa Idlib kutokana na uchafu wa magenge ya kigaidi, imewatia kiwewe waungaji mkono wa magaidi hao yaani nchi za Magharibi na hasa Marekani. Mkoa wa Idlib ndiyo ngome ya mwisho wa magenge ya kigaidi nchini Syria.
-
Russia yaionya Marekani isicheze na moto Syria
Aug 31, 2018 02:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia ameionya Marekani isicheze na moto huko Syria kwa kuchochea hujuma bandia ya silaha za kemikali ili kuhalalisha shambulizi dhidi ya wanajeshi wa Syria
-
Russia yaionya tena Marekani juu ya kufanya shambulizi dhidi ya Syria
Aug 30, 2018 11:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia ameelezea uwezekano wa Marekani na washirika wake kufanya shambulizi dhidi ya Syria hasa kwa kuzingatia hatua ya kusogezwa zana za kijeshi za nch hiyo katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Mawaziri wa Ulinzi wa Russia na Uturuki wajadili hali ya mambo Syria
Aug 30, 2018 11:21Mawaziri wa Ulinzi wa Russia na Uturuki wamefanya mazungumzo kuhusu hali ya mambo nchini Syria.
-
Magaidi wa DAESH (ISIS) wamenyonga zaidi ya watu elfu tano nchini Syria
Aug 30, 2018 03:24Kituo kiitwacho Uangalizi wa Haki za Binadamu nchini Syria kimeripoti kuwa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh limeua kwa kuwanyonga watu zaidi ya elfu tano nchini humo.
-
Russia: Magaidi nchini Syria wamejiandaa kufanya shambulio la silaha za kemikali
Aug 27, 2018 03:16Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Russia ametangaza kuwa magaidi walioko nchini Syria wamejiandaa kufanya shambulio la silaha za kemikali katika kipindi cha siku hizi mbili.