-
Marzouki alitaka jeshi la Tunisia kumuondoa madarakani rais wa nchi hiyo
Apr 11, 2022 11:29Rais wa zamani wa Tunisia, Moncef Marzouki ametoa wito kwa jeshi na vikosi vya usalama vya nchi hiyo kuingilia kati na kumwondoa madarakani rais wa sasa, Kais Saied na kulikabidhi mamlaka bunge lililochaguliwa na wananchi hadi pale uchaguzi mpya uliohuru na wa haki utakapofanyika.
-
Watoto 6 miongoni mwa wahajiri 13 waliokufa maji Tunisia
Apr 11, 2022 02:36Watoto 6 miongoni mwa wahajiri 13 waliokufa maji baada ya boti zao kuzama katika pwani ya Tunisia, wakijaribu kuelekea Italia.
-
Amnesty International yaitaka serikali ya Tunisia kukomesha "mashtaka ya kisiasa" dhidi ya wabunge
Apr 10, 2022 11:15Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa serikali ya Tunisia kukomesha manyanyaso ya kisiasa dhidi ya wabunge na kuheshimu haki na uhuru wao wa kujieleza, kukusanyika na kujumuika kwa amani.
-
Rais wa Tunisia aigiza Tume ya Uchaguzi iandae uchaguzi wa Bunge
Apr 05, 2022 11:52Rais wa Tunisia, Kais Saied ameitaka Tume Huru ya Uchaguzi nchini humo (ISIE) ifanye maandalizi ya uchaguzi wa Bunge uliopangwa kufanyika Disemba 17 mwaka huu.
-
Kuvunjwa Bunge la Tunisia
Apr 01, 2022 07:42Rais Kais Saied wa Tunisia amelivunja Bunge la nchi hiyo kufuatia kushtadi mivutano ya kisiasa nchini humo.
-
Rais Kais Saied wa Tunisia avunja Bunge, asema kuna jaribio la mapinduzi
Mar 31, 2022 03:12Rais wa Tunisia, Kais Saied jana Jumatano alitangaza kuvunja Bunge muda mfupi baada ya bunge hilo kupitisha sheria ya kufuta hatua za dharura zilizotangazwa na kiongozi huyo majira ya joto mwaka jana.
-
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tunisia anusurika kuuawa na magaidi
Mar 27, 2022 08:00Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tunisia, Taoufik Charfeddine amenusurika kuuawa katika shambulio linaloaminika kuwa la kigaidi.
-
Miili 20 ya wahajiri yaopolewa baharini pwani ya Tunisia
Mar 20, 2022 07:40Wapiga mbizi na maafisa usalama wa Tunisia jana Jumamosi waliopoa miili ya watu wengine wanane baada ya boti yao kuzama katika pwani ya nchi hiyo, na kufikisha idadi ya maiti zilizoopolewa hadi sasa kufikia 20.
-
Wanachama wa genge moja la kigaidi watiwa mbaroni nchini Tunisia
Mar 16, 2022 13:54Askari usalama nchini Tunisia wametangaza kuwa, wamefanikiwa kusambaratisha mtandao mmoja wa kigaidi ujulikanao kwa jila la "al Muwahhidun" katika miji wa Tataouine na Soussa ya kusini mwa mji mkuu Tunis.
-
Hatua ya Rais wa Tunisia kurefusha hali ya hatari yapokewa kwa hisia tofauti
Feb 20, 2022 02:49Wananchi wa Tunisia wamegawanyika baada ya Rais Kais Saied wa nchi hiyo kutangaza kurefusha muda wa hali ya hatari katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika hadi mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka huu wa 2022.