-
Gebran Bassil: Jumuiya ya Nchi za Kiarabu inapaswa kutofautisha baina ya muqawama na ugaidi
Nov 25, 2017 12:40Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Lebanon ameamwandikia barua Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) akimwambia kwamba, umoja huo unapaswa kufungamana na makubaliano ya Waarabu ambayo yalitofautisha baina ya muqawama na ugaidi.
-
Iran: Afrika isigeuzwe kimbilio la magenge ya kigaidi na ukufurishaji
Nov 24, 2017 12:25Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitizia udharura wa kufanyika jitihada za kuzuia bara la Afrika kugeuka kuwa kimbilio na kitovu cha magenge ya kigaidi na yenye misimamo ya kufurutu ada, kufuatia kusambaratishwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika nchi za Syria na Iraq.
-
Rais wa Russia akutana na Rais wa Syria na kumpongeza kufuatia mafanikio dhidi ya magaidi
Nov 21, 2017 04:38Rais Vladimir Putin wa Russia amempongeza Rais Bashar al-Assad wa Syria kufuatia ushindi mkubwa wa jeshi la Syria dhidi ya magaidi.
-
Hizbullah: Marekani imeisadia Daesh huko al Bukamal
Nov 21, 2017 00:09Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa Marekani imeilisaidia kundi la kigaidi la Daesh katika mapigano ya hivi majuzi katika mji wa al Bukamal nchini Syria hatua ambayo inakadhibisha madai ya Washington kwamba inapambana na ugaidi
-
Guterres aonya juu ya kutumiwa vibaya mapambano dhidi ya ugaidi
Nov 17, 2017 13:18Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kuhusu athari mbaya za sera za kupambana na ugaidi za baadhi ya nchi kwa suala la haki za binadamu.
-
Sisitizo la Senegal juu ya kudhaminiwa usalama katika nchi za bara la Afrika
Nov 14, 2017 08:33Katika kikao cha nne cha Kongamano la Amani na Usalama wa Afrika Rais Macky Sall wa Senegal amesisitizia ulazima wa kutolewa misaada kwa ajili ya kudhaminiwa usalama wa nchi za bara hilo.
-
Iran: Wanawake ndio wahanga wakuu wa magenge ya kigaidi
Oct 28, 2017 04:36Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema wanawake ndio wahanga wakuu wa ukatili wa makundi ya kigaidi duniani.
-
Watu saba wauawa katika hujuma ya kigaidi karibu na Mogadishu, Somalia
Oct 22, 2017 10:25Watu wasiopungua saba, wengi wakiwa wanawake wakulima, wameuawa karibu na mji mkuu wa Somalia kufuatia hujuma ya kigaidi huku mji huo ukiwa bado unaomboleza shambulizi la hivi karibuni lililoua mamia ya watu.
-
Magaidi wavunja benki na kushambulia kanisa Misri, 7 wauawa
Oct 16, 2017 10:28Kwa akali watu saba wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya genge moja la kigaidi kuvamia benki na kuiba, sambamba na kushambulia kanisa katika eneo la Sinai, kaskazini mwa nchi.
-
Siku za kundi la kigaidi la Daesh nchini Iraq zaanza kuhesabika
Oct 11, 2017 23:16Sambamba na ushindi wa kila siku wa jeshi la Iraq na makundi ya kujitolea ya wananchi katika mapambano ya kuliangamiza kundi la kigaidi la ِِِDaesh na kusafisha kabisa maeneo yote ya nchi hiyo, Waziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi ametangaza kuwa, kundi hilo litashindwa kikamilifu hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.