-
Jeshi la Uganda laua waasi zaidi ya 100 wa ADF Kongo DR
Dec 28, 2017 01:11Jeshi la Uganda limetangaza habari ya kuua wanachama wasiopungua 100 wa kundi la waasi wa ADF katika makabiliano makali yaliyojiri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Maelfu ya wakimbizi wa Kongo wawasili Uganda
Dec 27, 2017 23:13Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa limetangaza kuwa kuanzia tarehe 18 mwezi huu hadi hivi sasa zaidi ya wakimbizi 4500 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekimbilia Uganda.
-
Uganda na DRC kushirikiana katika kupambana na waasi wa ADF
Dec 20, 2017 04:46Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimekubaliana kuimarisha utaratibu wa mawasiliano na kupeana taarifa za kiintelijensia kwa ajili ya kupambana na waasi wa ADF kufuatia mashambulizi yao dhidi ya vikosi vya walinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa.
-
Mbunge wa Kivu Kaskazini atahadharisha kuhusu vitisho vya waasi wa ADF-Nalu wa Uganda
Dec 11, 2017 04:38Juvenal Munubo, mwakilishi wa Kivu Kaskazini katika Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ametahadharisha kuhusiana na vitisho vya waasi wa ADF-Nalu wa Uganda wanaoendesha harakati zao mashariki mwa DRC.
-
Uchunguzi wa maoni: Asilimia 85 ya Waganda 'hawamtaki' Museveni
Dec 10, 2017 03:44Uchunguzi wa maoni umeonyesha kuwa asilimia 85 ya wananchi wa Uganda hawaungi mkono muswada wa kufanyia marekebisho katiba ili kuondoa kikomo cha umri wa kugombea urais.
-
Makumi ya wanajeshi wa Uganda waanza kuondoka Somalia
Dec 07, 2017 11:41Jeshi la Ulinzi la Uganda UPDF limeanza kuondoa makumi ya wanajeshi wake wanaohudumu ndani ya Kikosi cha Askari wa Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom.
-
Besigye akamatwa tena, polisi Uganda yatumia vitoa machozi kuzima mkutano wa upinzani
Nov 15, 2017 03:49Kwa mara nyingine tena polisi ya Uganda imemtia mbaroni kinara wa upinzani nchini humo Kizza Besigye, kwa tuhuma za kuitisha mkutano wa hadhara pasina kibali cha vyombo vya usalama.
-
Magufuli na Museveni walaani uamuzi wa ICC kuhusu Burundi
Nov 11, 2017 12:24Marais wa Tanzania na Uganda wamelaani uamuzi ulitolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), ambayo imemuagiza Mwendesha Mashtaka wake, Fatou Bensouda kuanzisha uchunguzi wa vitendo vya kihalifu dhidi ya binadamu vilivyotokea nchini Burundi.
-
WHO yatahadharisha kuhusu ugonjwa wa virusi vya Marburg Kenya na Uganda
Nov 11, 2017 12:23Shirika la Afya Duniani (WHO) limewatahadharisha wageni wanaotembelea Hifadhi ya Taifa ya Mt Elgon juu ya hatari ya kupatwa na ugonjwa wa virusi vya Marburg.
-
Madaktari Uganda wafanya mgomo wakidai nyongeza ya mishahara
Nov 07, 2017 23:26Madaktari wa Uganda wameanza mgomo wa nchi nzima baad ya serikali kushindwa kutekeleza matakwa yao kuhusu nyongeza ya mshahara na kuboresha mazingira ya kazi katika hospitali za umma.