-
Ripoti ya UN: RSF inashambulia na kuua raia Darfur, Sudan kwa msingi wa ukabila
Mar 01, 2024 23:38Ripoti mpya ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa imesema, Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF pamoja na wanamgambo vinaoshirikiana nao wanaopigania kutwaa madaraka nchini Sudan wamefanya mauaji ya kikabila na ubakaji wakati wa udhibiti wa eneo kubwa la Darfur magharibi mwa nchi hiyo, na kwamba vitendo hivyo vinaweza kuwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.
-
Afrika Kusini: UN iache undumakuwili katika kulaani ukiukwaji wa haki
Feb 27, 2024 03:59Afrika Kusini imekosoa vikali undumakuwili wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa katika suala la kulaani ukanyagaji wa haki za binadamu duniani.
-
Wataalamu wa UN: Kuipelekea silaha Israel kukomeshwe mara moja!
Feb 24, 2024 23:05Kundi la wataalamu wa Umoja wa Mataifa limeonya kwamba upelekaji wowote wa silaha au risasi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel ambazo zitatumika katika mashambulizi ya ardhini na angani dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghazza uliozingirwa unaweza ukawa unakiuka sheria za kimataifa za kibinadamu, na lazima ukomeshwe mara moja.
-
UN: Jeshi la Israel limewabaka, limewapiga vibaya na kuwanyima chakula na dawa wanawake Wapalestina
Feb 20, 2024 03:36Mamia ya wanawake na wasichana wa Kipalestina katika maeneo ya Ghazza na Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu wamekuwa wakiwekwa kizuizini kiholela na jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel tangu Oktoba 7, na kuripoti kuwa wamebakwa, kupigwa vibaya na kunyimwa chakula na dawa na askari wa jeshi hilo.
-
Umoja wa Mataifa: Idadi ya raia waliouawa huko Gaza haijawahi kushuhudiwa
Feb 15, 2024 23:13Mkuu wa Kitengo cha Asia Magharibi katika Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema: Idadi ya raia na waandishi wa habari waliouawa huko Gaza haina mfano.
-
Umoja wa Mataifa walaani njama za kuichafua UNRWA
Feb 06, 2024 22:52Maripota wa Umoja wa Mataifa wametangaza kuwa, wanalaani vikali jaribio lolote la kuharamisha na kulichafua Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).
-
Maripota wa Umoja wa Mataifa walaani njama za kuichafua UNRWA
Feb 05, 2024 12:13Maripota wa Umoja wa Mataifa wametangaza kwamba wanalaani vikali jaribio lolote la kuharamisha na kuchafua Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).
-
Abdollahian akosoa vikali mashambulio ya Marekani dhidi ya Syria na Iraq
Feb 04, 2024 03:57Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hujuma na mashambulio ya hivi karibuni ya Marekani katika mataifa ya Syria na Iraq chimbuko lake ni utendaji wa kimakosa na usio sahihi wa Washington katika kutatua matatizo ya Asia Magharibi kwa ktumia mtutu wa bunduki.
-
UN yailaani Israel kwa kuwaua na kuwanyamazisha waandishi wa habari huko Gaza
Feb 02, 2024 10:36Wataalamu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza kusitikishwa na kulaani vitendo vya waandishi wa habari kuuawa, kushambuliwa, kujeruhiwa na kuwekwa vizuizini na vikosi vya utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu la Ukanda wa Gaza.
-
Umoja wa Mataifa washtushwa na mauaji ya watu 50 nchini Mali
Feb 02, 2024 04:19Mkuu wa Ofisi ya Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kusikitishwa na mauaji ya karibuni ya makumi ya watu nchini Mali.