-
UN: Watu wa Gaza wanapambana kila siku ili kuishi
Feb 01, 2024 23:10Umoja wa Mataifa umesema kuwa wakazi wa Kipalestina wa Ukanda wa Gaza kila siku wanapambana ili kuweza kuishi.
-
UN: Maelfu ya Wapalestina wa Gaza waliokamatwa na askari wa Israel wanateswa
Jan 20, 2024 03:52Umoja wa Mataifa umesema huenda vikosi vya jeshi la Israel vimewakamata maelfu ya Wapalestina wakazi wa Ukanda wa Gaza, huku utawala huo wa Kizayuni ukiendeleza mauaji na jinai za kutisha dhidi ya wakazi wa eneo hilo uliolizingira.
-
Mapigano ya kikabila yameua zaidi ya 15,000 katika mji mmoja Sudan
Jan 20, 2024 03:51Ripoti ya Umoja wa Mataifa imesema watu kati ya 10,000 na 15,000 waliuawa katika ghasia na mapigano ya kikabila mwaka jana katika mji mmoja ulioko katika jimbo la Darfur Magharibi nchini Sudan.
-
Mtaalamu wa UN: Hakuna kinachoweza kuhalalisha ilichokifanya Israel Gaza
Jan 19, 2024 08:17Mtalaamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ameashiria ukiukaji wa sheria za kimataifa uliofanywa mara chungu nzima na utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, hakuna kitu kinachoweza kuhalalisha vita vya mauaji ya kimbari vya Israel katika eneo hilo lilozingirwa.
-
Guterres asisitiza udharura wa kufanyika marekebisho katika Umoja wa Mataifa
Jan 18, 2024 00:12Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza haja ya kufanyika marekebisho katika muundo wa Baraza la Usalama la shirika hilo la kimataifa.
-
OCHA: Israel inazuia kupelekwa dawa kaskazini mwa Gaza
Jan 16, 2024 23:06Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kuzuia ufikishaji wa misaada muhimu ya kibinaadamu ikiwa ni pamoja na dawa muhimu na mafuta ya kuendesha huduma za maji na usafi wa mazingira kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.
-
UN: "Siku 100 za mashambulizi ya Israel huko Gaza zinahisika kama miaka 100" kwa Wapalestina
Jan 15, 2024 01:03Philippe Lazzarini, Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), amesema siku 100 zilizopita za mashambulizi ya Israel huko Ukanda wa Gaza zimekuwa kama miaka 100 kwa watu wa Gaza.
-
UN yatiwa wasiwasi na kuongezeka kauli za chuki za kikabila DRC, yataka hatua zichukuliwe
Jan 08, 2024 02:40Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk amesema ana wasiwasi mkubwa kutokana na kuongezeka kwa kauli za chuki zenye misingi ya kikabiila na uchochezi wa ghasia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC.
-
Umoja wa Mataifa: Vita vya Gaza lazima vikomeshwe
Jan 07, 2024 07:44Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na Masuala ya Kibinadamu Martin Griffiths amesema ni lazima Jamii ya Kimataifa itumie "ushawishi wake wote" kumaliza vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu UN yasisitiza tena: Ni marufuku kuwalazimisha watu wa Gaza kuhama nchi yao
Jan 05, 2024 03:26Kamishna Mkuu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa amepinga matamshi yaliyotolewa na viongozi wa serikali ya Israel kuhusu suala la kuwahamisha watu wa Ukanda wa Gaza na kuwapeleka katika nchi zingine.