-
UN: Watu milioni 38 wanaishi na HIV, Ukimwi umeua 770,000, 2018
Dec 01, 2019 04:09Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema watu milioni 38 kote duniani wanaishi na virusi hatari vya HIV, huku ugonjwa wa Ukimwi unaosababishwa na virusi hivyo ukiua watu 770,000 mwaka jana 2018.
-
UN: Sudan Kusini yasajili kikosi kipya cha wapiganaji kinyume na makubaliano
Nov 27, 2019 10:06Umoja wa Mataifa umesema Idara ya Usalama wa Taifa ya Sudan Kusini imeunda kikosi kipya chenye wapiganaji 10,000 kinyume na makubaliano ya amani.
-
Iran: Baraza la Usalama la UN linakabiliwa na migogoro ya uhalali na itibari, linahitaji mageuzi
Nov 26, 2019 04:36Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema, Baraza la Usalama la umoja huo linakabiliwa na migogoro ya uhalali na itibari ambayo inapasa ishughulikiwe kwa kufanyiwa mageuzi baraza hilo.
-
UN: Thuluthi moja ya wanawake wanakabiliwa na dhulma za kijinsia
Nov 25, 2019 08:42Umoja wa Mataifa umesema katika kila wanawake watatu, mmoja amekabiliwa na dhulma za kijinsia au kunajisiwa.
-
Jumuiya za kimataifa zapinga uteuzi wa Ghada Wali kuwa Mkurugenzi wa UNODC
Nov 24, 2019 23:22Jumuiya za kimataifa za kutetea haki za binadamu zimepinga uteuzi uliofanywa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na kumtangaza Ghada Wali, Waziri wa Ustawi za Jamii wa Misri kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Mihadarati na Jinai (UNODC).
-
Wanachama wa Baraza la Usalama waikosoa vikali Marekani
Nov 22, 2019 23:08Rais Donald Trump wa Marekani amechukua msimamo wa kuunga mkono kwa hali na mali na bila ya masharti yoyote utawala haramu wa Israel na licha ya maazimio kadhaa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanayopiga marufuku kuunganishwa ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo tokea mwaka 1967, ikiwemo miinuka ya Golan ya Syria, lakini bado serikali ya Washington inauchukulia ukaliaji mabavu huo wa utawala wa Kizayuni kuwa ni jambo halali na linaloruhusiwa.
-
UN: Nusu ya waathriwa wa vita vya Yemen ni wanawake na watoto
Nov 21, 2019 00:11Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu nchini Yemen imetangaza kupitia taarifa kwamba, nusu ya waathiriwa wa vita vya nchi hiyo ni wanawake ni watoto.
-
UN: Watoto milioni 7 wapo kizuizini, Marekani yaongoza
Nov 20, 2019 04:09Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa imebainisha kuwa, watoto zaidi ya milioni saba wanashikiliwa katika jela na vituo mbalimbali duniani, huku Marekani ikiongoza katika orodha hiyo.
-
Zarif: EU haijachukua hatua yoyote ya maana ya kulinda JCPOA
Nov 12, 2019 04:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezikosoa nchi za Ulaya kwa kuakhirisha ahadi zao na kufeli kufungamana na mapatano ya nyuklia ya JCPOA, huku zikiitaka Tehran ifungamane kikamilifu na makubaliano hayo.
-
UN yakaribisha kuongezwa muda wa kipindi cha mpito Sudan Kusini
Nov 12, 2019 04:31Umoja wa Mataifa umekaribisha uamuzi wa Shirika la Kiserikali la Ustawi wa nchi za Mashariki mwa Afrika (IGAD) wa kurefusha kwa siku 100 kipindi cha mpito nchini Sudan Kusini.