-
UN: Magaidi elfu 30 wa kundi la Daesh wangali hai
Jul 30, 2019 06:34Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh elfu 30 wangali hai.
-
Russia yawasilisha mpango wa usalama wa Ghuba ya Uajemi kwa Umoja wa Mataifa
Jul 30, 2019 06:24Uwepo wa kijeshi wa nchi za kigeni katika eneo la Ghuba ya Uajemi na taathira zake mbaya ambazo zimepelekea kuongezeka mivutano ya kisiasa na kijeshi katika eneo, umeipelekea Russia kuwasilisha mpango wa usalama wa eneo hili la kistratijia kwa Umoja wa Mataifa.
-
Ansarullah ya Yemen: Marekani na Umoja wa Mataifa zinachangia jinai za Saudi Arabia
Jul 30, 2019 02:46Harakati ya Ansarullah ya Yemen imetangaza kuwa, serikali ya Marekani na Umoja wa Mataifa zinabeba jukumu la jinai zinazofanywa na muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia.
-
Al-Sarraj na UN wasisitiza udharura wa kuanza tena mchakato wa kisiasa Libya
Jul 28, 2019 23:48Waziri Mkuu wa Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya na mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya wametilia mkazo udharura wa kuanzishwa tena mchakato wa kisiasa nchini humo.
-
Katibu Mkuu wa UN: Ubomoaji nyumba za Wapalestina si halali kisheria
Jul 26, 2019 02:56Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, anatiwa wasiwasi na ubomoaji nyumba za Wapalestina unaofanywa na utawala wa Kizayuni na kusisitiza kuwa, sera za Israel za kuharibu na kuteketeza mali za Wapalestina haziendani na sheria za kimataifa.
-
UN yakosoa vizingiti vya utawala wa Trump dhidi ya Zarif
Jul 16, 2019 03:19Umoja wa Mataifa umekosoa vikali hatua ya utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani ya kumwekea vizingiti Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Javad Zarif.
-
UN: Watu milioni 821 wanakabiliwa na njaa duniani
Jul 16, 2019 02:48Umoja wa Mataifa umesema watu zaidi ya milioni 821 katika pembe mbalimbali za dunia wanakabiliwa na baa la njaa; mwaka jana 2018 ukiwa mwaka wa tatu mfululizo kwa idadi hiyo kuongezeka kwa kiwango cha kutisha.
-
Hofu ya UN kuhusu kushtadi migogoro katika majimbo ya Somalia
Jul 09, 2019 03:52Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu kuongezeka migogoro na mivutano baina ya majimbo yenye mamlaka ya ndani nchini Somalia kwa upande mmoja, na majimbo hayo na serikali kuu ya Mogadishu kwa upande mwingine.
-
Jeshi la Sudan Kusini lakanusha madai ya UN kuwa limeua raia
Jul 04, 2019 21:56Jeshi la Sudan Kusini limekanusha vikali madai ya Umoja wa Mataifa kwamba limeua makumi ya raia wa nchi hiyo katika eneo la Central Equatoria.
-
Marekani yakwamisha azimio la Baraza la Usalama kuhusu mauaji ya wahajiri Libya
Jul 04, 2019 03:02Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilimaliza kikao chake cha faragha jana jioni kwa wakati wa New York kuhusiana na Libya bila ya kuafikiana mwafaka kuhusu shambulizi la anga lililolenga makazi ya wahajiri katika eneo la Tajoura huko mashariki mwa Tripoli ambalo limeua wakimbizi 60 na kujeruhi wengine zaidi ya 130.