-
UNICEF yatoa indhari: Kizazi cha Waislamu Warohingya wa Myanmar kinakabiliwa na hatari ya kutoweka
Aug 23, 2018 10:30Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF limetahadharisha kuwa kizazi cha Waislamu Warohingya walioko nchini Myanmar na kwenye kambi za wakimbizi kwenye mpaka wa Bangladesh kinakabiliwa na hatari ya kutoweka.
-
UNICEF: Kila mwaka watoto 66 elfu wa Yemen wanafariki dunia kwa maradhi yanayozuilika
Aug 16, 2018 02:57Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto (UNICEF) umesema kuwa, watoto 66 elfu wenye umri wa chini ya miaka mitano wanafariki dunia nchini Yemen kila mwaka kutokana na maradhi yanayozuilika.
-
UNICEF: Saudia iache kushambulia miundombinu ya Yemen
Aug 01, 2018 21:58Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa Unicef, umeutaka utawala wa Aal-Saud, ukomeshe mashambulizi yake dhidi ya miundombinu ya Yemen.
-
Indhari ya Unicef kuhusu hali ya mgogoro huko Yemen
Jul 18, 2018 22:36Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umetangaza kuwa kuendelea mapigano huko Yemen kunazifanya ngumu shughuli za utoaji misaada ya kibinadamu nchini humo.
-
UN: Watoto milioni 30 wamepoteza makao kutokana na vita
Jun 19, 2018 22:13Takribani watoto milioni 30 wampoteza makao yao duniani kutokana na vita na sasa wanahitaji ulinzi pamoja na suluhu endelevu kwa ajili ya mustakbali wao.
-
UNICEF: Watoto wengi waliokuwa jeshini Sudan Kusini wameachiliwa huru
Apr 20, 2018 02:51Watoto zaidi ya 200 waliokuwa wamesajiliwa kama wanajeshi katika makundi ya wapiganaji nchini Sudan Kusini wameachiliwa huru.
-
Indhari ya Unicef kuhusu hali mbaya ya watoto nchini Syria
Mar 14, 2018 23:55Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umetahadharisha kuhusu hali mbaya inayowakabili watoto huko Syria.
-
Pakistan, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Afghanistan ni nchi hatari zaidi kuzaliwa mtoto
Feb 20, 2018 23:43Idadi kubwa ya watoto wanapoteza maisha punde wanapozaliwa katika maeneo ya kati na magharibi mwa Afrika licha ya kuwa afya ya mtoto imeboreka kiujumla duniani, imesema Idara ya Umoja wa Mataifa ya Kuhudumia Watoto, UNICEF.
-
UNICEF yatahadharisha kuhusu kutumiwa watoto kama askari vitani
Feb 12, 2018 23:29Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetahadharisha kuhusiana na suala la kutumiwa watoto kama askari vitani katika maeneo mbalimbali duniani.
-
Wasiwasi wa Unicef kuhusu hali ya watoto wa Kiiraqi
Feb 12, 2018 10:58Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa mtoto mmoja wa Kiiraqi kati ya wanne nchini humo anaishi katika hali ya umaskini na kwamba Wairaqi wengine milioni nne wanahitaji msaada ikiwa ni natija ya kujiri vita vya kundi la kigaidi la Daesh huko Iraq.