-
Katibu Mkuu wa UN: Mahesabu mabaya Asia Magharibi yatasababisha janga kwa dunia
Apr 19, 2024 23:29Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kuhusu hali ya sasa katika eneo la Asia Magharibi na kusisitiza kuwa, kosa moja la kimahesabu yumkini likasababisha maafa kwa eneo hilo na dunia nzima kwa ujumla.
-
Utawala wa Kizayuni una hofu ya kutolewa waranti wa kumkamata Netanyahu
Apr 19, 2024 03:59Baraza la Mawaziri la utawala wa Kizayuni limefanya kikao cha dharura kuchunguza uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kutoa waranti wa kukamatwa Benjamin Netanyahu na maafisa wengine wa utawala huo dhalimu wa Israel kwa kuhusika na mauaji ya kimbari ya Wapalestina huko Ghaza.
-
Kukiri Pentagon kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran katika kuujibu utawala wa Kizayuni
Apr 18, 2024 08:49Patrick Ryder Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri juu ya nguvu za kijeshi za Iran katika kutoa jibu la kijeshi kwa utawala wa Israel.
-
UN: Israel inaendeleza vikwazo haramu vya misaada kwa watu wa Gaza
Apr 18, 2024 07:30Msemaji na Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa utawala haramu wa Israel unaendeleza vikwazo visivyo halali vya katika uwanja wa kupeleka misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza.
-
Wawakilishi wa Kongresi: Israel inakiuka sheria kwa kutumia silaha za Marekani kufanya mauaji
Apr 18, 2024 07:10Kundi la wawakilishi wa chama cha Demokratic katika Kongress ya Marekani limesisitiza kuwa, utawala wa Israel unakiuka sheria kwa kutumia silaha za Marekani kufanya mauaji na mashambulizi makali huko Palestina.
-
Kujitetea kwerevu kwa Iran kwa ajili ya Gaza
Apr 17, 2024 08:11Hatua ya Iran kujitetea kihalali dhidi ya shambulio la kichokozi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wake nchini Syria, ambayo ilifanyika kwa utaratibu wa hali ya juu na kupitia silaha tofauti za mashambulio, imekuwa na athari na matokeo ya kieneo na kimataifa angalau imepelekea wakaazi wa Gaza kupata usiku mmoja wa amani na utulivu.
-
Rais Raisi: Operesheni ya "Ahadi ya Kweli" ilikuwa hatua ya kiwango maalumu na ya kuwatia adabu tu Wazayuni
Apr 17, 2024 07:41Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Operesheni ya Ahadi ya Kweli ilikuwa hatua ya kiwango maalumu na ya kuutia adabu tu utawala wa Kizayuni na akasisitiza kwamba, endapo utawala huo utafanya uchokozi mdogo kabisa dhidi ya ardhi ya Iran utakabiliwa na jibu kali zaidi na la nguvu kubwa zaidi.
-
Wapalestina 16 wa Ukanda wa Ghaza wameuawa shahidi kwenye jela za utawala wa Kizayuni
Apr 17, 2024 07:19Kamati inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa na walioachiwa huru kutoka kwenye magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa, mateka 16 wakazi wa Ukanda wa Ghaza wameuawa shahidi wakiwa wanashikiliwa kwenye magereza ya utawala huo.
-
Amir-Abdollahian: Mgogoro wa Asia Magharibi umesababishwa na mashambulizi ya Israel
Apr 17, 2024 03:17Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan na kusisitiza kuwa, mgogoro uliopo katika eneo la Asia Magharibi hivi sasa umesababishwa na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Kikao cha Baraza la Usalama: Uwanja wa makabiliano kati ya waungaji mkono wa Iran na Wamagharibi wanaounga mkono utawala wa Kizayuni.
Apr 16, 2024 04:24Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujadili mashambulizi ya Iran ya kuuadhibu utawala wa Israel kilifanyika Jumapili jioni tarehe 14 Aprili, kikao ambacho kilibadilika na kuwa uwanja wa makabiliano kati ya nchi zinazounga mkono Iran na kambi ya Magharibi waitifaki wa utawala wa Kizayuni.