-
Al Nujaba: Harakati za Uturuki nchini Iraq ni tishio
Mar 07, 2022 08:40Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya nchini Iraq ya al Nujaba amesema kuwa harakati za Uturuki huko Iraq ni tishio; na kwamba iwapo nchi hiyo haitaacha chokochoko zake hizo basi Wairaki wataingia katika hali ya kijeshi.
-
Kumairishwa ushirikiano wa kiusalama na kiintelijinsia kati ya Uturuki na Israel
Feb 17, 2022 23:14Mgogoro wa kiuchumi na matatizo ya kifedha yanayoikabili Uturuki yameendelea kugonga vichwa vya habari katika magazeti ya nchi hiyo.
-
Erdogan: Rais wa Israel ataitembelea Uturuki mwezi ujao
Feb 03, 2022 09:07Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema rais wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel, Isaac Herzog ataitembelea nchi hiyo mwezi ujao wa Machi.
-
Khazali: Wanamuqawama wa Iraq watajibu uchokozi mpya wa Uturuki
Feb 02, 2022 23:00Katibu Mkuu wa harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq ambalo ni tawi la muungano wa makundi ya muqawama wa Hashd al-Sha’abi nchini Iraq amesisitiza kuwa, mrengo wa mapambano ya Kiislamu utatoa jibu mwafaka kwa uvamizi na chokochoko mpya za jeshi la Uturuki dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Watu wanane wameuawa na kujeruhiwa katika mashambulizi ya ndege za kivita za Uturuki kaskazini mwa Iraq
Feb 02, 2022 04:27Vyombo vya habari vimetangaza kuwa watu wasiopungua wanane wameuawa na kujeruhiwa katika mashambulizi ya ndege za kivita za Uturuki katika mji wa Sinjar kaskazini mwa Iraq.
-
Pakistan, Uturuki na Malaysia kuasisi televisheni ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu
Dec 20, 2021 05:42Waziri wa Habari na Turathi za Taifa wa Pakistan amesema, nchi hiyo kwa kushirikiana na Uturuki na Malaysia zitaanzisha chaneli ya televisheni kwa lengo la kukabiliana na kampeni za uenezaji chuki dhidi ya Uislamu duniani.
-
Raisi: Uhusiano wa Iran na Uturuki utaingia katika marhala mpya
Dec 09, 2021 01:00Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria umuhimu wa uhusiano wa kiuchumi na kibiashara wa Tehran na Ankara na kusema kuwa, kustawi kwa ushirikiano wa pande mbili kutaingia katika hatua mpya karibuni hivi, kwa kufanyika kongamano hapa Tehran.
-
Safari ya mrithi wa ufalme wa Imarati nchini Uturuki; sababu na malengo yake
Nov 25, 2021 04:07Mohammed Bin Zayed Al Nayhan, mrithi wa ufalme wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) jana Jumatano tarehe 24 Novemba aliwasili mjini Ankara, Uturuki ambapo alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Recep Tayyip Erdoğan wa nchi hiyo.
-
Niger kununua silaha na zana za kijeshi kutoka Uturuki
Nov 20, 2021 23:32Niger na Uturuki zimetangaza kufikia makubaliano ambayo yanajumuisha kuiuzia Niger silaha mbalimbali zikiwemo ndege zisizo na rubani (droni) na magari ya kivita ili kuongeza uwezo wake wa kijeshi katika kukabiliana na makundi ya kigaidi.
-
Amir-Abdolahian: Iran na Uturuki ni nchi mbili kubwa katika eneo na mchango wao haupingiki
Nov 16, 2021 23:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa ripoti kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram kuhusu mazungumzo yake na waziri mwenzake wa Uturuki hapa Tehran na kusema kuwa, Iran na Uturuki ni nchi mbili kubwa katika eneo la Asia Magharibi na mchango wa nchi hizo mbili katika eneo hilo haukanushiki.