Aug 14, 2017 08:52
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa vitisho vya kutumia nguvu za jeshi vilivyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya Venezuela na kusisitiza kuwa uzoefu unaonesha kuwa, zama za kutumia vitisho vya kijeshi na mashinikizo dhidi ya nchi huru na zinazojitawala kwa ajili ya kuzilazimisha zikubali matakwa yasiyo ya kimantiki na haramu zimemalizika.