-
Somalia yakataa "rushwa" ya Saudia, yagoma kujiunga na nchi zinazoisusia Qatar
Aug 30, 2017 22:23Rais wa Somalia amekataa pendekezo la kupewa Euro milioni 68 lililotolewa na utawala wa Kifalme wa Saudi Arabia mkabala wa kujiunga na muungano wa nchi zilizokata uhusiano wao na kuisusia Qatar.
-
Nchi za Ulaya zaendelea kupinga vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Russia
Aug 10, 2017 23:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Sigmar Gabriel amesema kuhusu vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Russia kwamba, hatua mpya za Marekani za kutaka kuibana zaidi Russia zinaweza kusababisha matatizo katika umoja wa nchi za Magharibi kuhusu mgogoro wa Ukraine.
-
Kutekelezwa vikwazo mpya vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Russia
Aug 06, 2017 23:14Umoja wa Ulaya umeanza kutekeleza vikwazo vipya dhidi ya Russia kuhusiana na mzozo wa peninsula ya Crimea.
-
Araqchi: Vikwazo vipya vya US vinalenga kuisambaratisha JCPOA
Aug 03, 2017 02:55Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani kusaini sheria ya vikwazo vipya dhidi ya Tehran ni njama ya Washington ya kutaka kusambaratisha makubaliano ya nyuklia ya Vienna yanayojulikana kwa kifupi kama JCPOA.
-
Trump asaini mswada wa vikwazo dhidi ya Iran, Russia na Korea Kaskazini
Aug 02, 2017 22:04Rais Donald Trump wa Marekani amesaini kuwa sheria mpango wa vikwazo uliopitishwa na Bunge la Wawakilishi na Seneti ya nchi hiyo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Russia na Korea Kaskazini.
-
Nchi nne za Kiarabu zang'ang'ania msimamo wao wa kuendeleza vikwazo dhidi ya Qatar
Jul 30, 2017 23:57Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi nne za Kiarabu zilizovunja uhusiano wa kidiplomasia na Qatar na kuiwekea vikwazo nchi hiyo wametoa taarifa wakitilia mkazo misimamo ya hapo kabla ya nchi hizo na kuendelezwa vikwazo dhidi ya Doha.
-
Russia yajibu Marekani, yapunguza idadi ya wanadiplomasia wa Marekani na kuzuia mali zao
Jul 28, 2017 21:51Katika kujibu hatua ya vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Russia, serikali ya Moscow imetoa amri ya kupunguzwa idadi ya wanadiplomasia wa nchi hiyo nchini humo sambamba na kuzuia baadhi ya mali za kidiplomasia za maafisa hao.
-
Syria yakosoa kuendelezwa vikwazo vya nchi za Magharibi dhidi yake
Jul 28, 2017 21:51Bashar Jaafari, Mwakilishi wa Kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amelaani mwendelezo wa vikwazo vya kidhalimu vya nchi za Magharibi dhidi yake na kusema kwamba vikwazo hivyo vimelemaza kabisa shughuli za mashirika ya misaada ya kibinadamu nchini humo.
-
Kamal Kharrazi: Hatua za kihasama za Marekani dhidi ya Iran si jambo jipya
Jul 28, 2017 02:59Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Uhusiano wa Nje wa Iran amesema: Hatua za kihasama za Rais wa Marekani dhidi ya Iran ni siasa zilizoanza tangu mwaka 1979 wakati wa ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na zinaendelea hadi sasa.
-
Dakta Larijani: Iran imejiandaa kukabiliana na vikwazo vipya vya Marekani
Jul 27, 2017 23:03Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Iran imejiandaa kikamilifu kukabiliana na vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya taifa hili.