-
Libya yaanzisha uchunguzi kuhusu biashara ya utumwa
Nov 20, 2017 02:48Naibu Mkuu wa Baraza la Uongozi la Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya amesema kuwa wameanzisha uchunguzi kuhusu suala la kushikiliwa na kuuzwa wahajiri kama watumwa karibu na mji mkuu wa nchi hiyo, Tripoli.
-
Wahajiri 73 wapoteza maisha katika fukwe za Libya
Nov 08, 2017 07:47Wahajiri 73 wamekufa maji katika bahari ya Mediterranean wakati walipokuwa wanajaribu kuzifikia fukwe za Italia kutokea Libya.
-
Wahajiri wa Kiafrika wazidi kufa maji wakielekea Ulaya kutafuta maisha
Nov 07, 2017 08:20Kwa akali wahajiri watano wa Kiafrika wamefariki dunia baada ya boti yao kuzama katika bahari ya Mediterranean, magharibi mwa pwani ya Libya.
-
Angola yawatimua maelfu ya wahamiaji haramu wa Kongo DR
Nov 06, 2017 02:46Serikali ya Angola imewafukuza nchini humo maelfu ya wahamiaji haramu raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Askari wa gadi ya pwani nchini Italia waokoa wahajiri 700
Nov 04, 2017 07:48Askari wa gadi ya pwani nchini Italia wametangaza kwamba Ijumaa ya jana waliwaokoa wahajiri 700 katika bahari ya Mediterranea.
-
Wahajiri 900 waokolewa, 7 wafa maji katika pwani ya Libya
Nov 02, 2017 08:10Miili saba ya wahajiri haramu imepatikana ndani ya boti ya plastiki karibu na pwani ya Libya, huku mamia ya wengine wakiokolewa kusini mwa bahari ya Mediterranean.
-
Wahajiri zaidi ya elfu 3 wakamatwa Libya
Oct 08, 2017 14:17Serikali ya Libya imewatia mbaroni maelfu ya wahajiri haramu katika mji wa Sabratha, kaskazini magharibi mwa nchi, ikiwa ni katika jitihada za kupambana na magendo ya binadamu.
-
Wahajiri 140 waokolewa baada ya boti zao kuzama Tunisia
Oct 01, 2017 15:15Jeshi la Majini la Tunisia limefanikiwa kuokoa wahajiri wapatao 140, baada ya boti zao kuzama kusini mashariki mwa nchi.
-
Jeshi la wanamaji Libya: Tumeokoa zaidi ya wahajiri 3000 ndani ya kipindi cha wiki moja
Sep 18, 2017 07:22Msemaji wa kikosi cha jeshi la wanamaji nchini Libya amesema kuwa, askari wa gadi ya pwani ya nchi hiyo wamefanikiwa kuokoa zaidi ya wahajiri haramu 3000 ndani ya kipindi cha wiki moja katika bahari ya Mediterranean.
-
Viwiliwili vya wahajiri 16 vyapatikani jangwani mashariki mwa Libya
Sep 06, 2017 07:10Vikosi vya usalama nchini Libya vimetangaza habari ya kupatikana miili 16 ya wahajiri katika eneo la jangwani, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Misri.