-
Wanachuo Zimbabwe waandamana dhidi ya Mugabe
Nov 20, 2017 11:06Wanachuo nchini Zimbabwe wamefanya maandamano katika kuonyesha upinzani wao kwa rais wa nchi hiyo.
-
Mugabe akataa tena kujiuzulu
Nov 19, 2017 23:58Licha ya hapo awali kutangazwa kuwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amekubali kujiuzulu na kwamba angeliitumia hotuba yake kwa taifa kutangaza rasmi kuachia madaraka, lakini rais huyo kizee hakusema chochote kuhusiana na kujiuluzu kwake wakati alipolihutubia taifa jana usiku.
-
Duru za ZANU-PF: Chama tawala Zimbabwe kinapanga kumtimua Mugabe
Nov 19, 2017 04:40Viongozi wa chama tawala nchini Zimbabwe cha ZANU-PF wanatazamiwa kupitisha uamuzi wa kumuondoa uongozini Rais wa nchi hiyo na kiongozi wa chama hicho Robert Gabriel Mugabe, ambaye amekuwa akiiongoza nchi hiyo tangu ilipopata uhuru wake miaka 37 iliyopita. Hayo ni kwa mujibu wa duru mbili kutoka ndani ya chama hicho.
-
Muswada wa kumsaili Mugabe, wawasilishwa katika bunge la Zimbabwe
Nov 19, 2017 00:59Mpango wa kusailiwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe umewasilishwa katika bunge la nchi hiyo.
-
Maelfu waandamana Zimbabwe wakishinikiza Mugabe ajiuzulu
Nov 18, 2017 11:27Maelfu ya raia wameandamana leo nchini Zimbabwe hasa katika mji mkuu Harare wakiunga mkono hatua ya jeshi ya kumuondoa madarakani Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo na kupiga nara wakishinikiza kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 ajiuzulu na kuachia madaraka ya nchi.
-
Mugabe azidi kukabiliwa na mashinikizo ya kujiuzulu, Rais wa Botswana amkosoa, maandamano dhidi yake yafanyika Harare
Nov 18, 2017 04:12Rais Ian Khama wa Botswana amemtaka Rais mkongwe wa Zimbabwe Robert Mugabe aachie madaraka akisisitiza kuwa kiongozi huyo hana uungaji mkono wa kidiplomasia wa kieneo wa kumfanya abaki madarakani.
-
Chama tawala nchini Zimbabwe kuongoza maandamano dhidi ya Mugabe
Nov 17, 2017 23:50Chama tawala nchini Zimbabwe Zanu-PF hii leo klnatazamiwa kuongoza maandamano katika mji mkuu Harare, kumshinikiza Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo ajiuzulu.
-
Chama tawala Zimbabwe chasema hakuna kurudi nyuma, Mugabe ang'atuke
Nov 17, 2017 13:21Chama tawala nchini Zimbabwe cha Zanu- PF kimetangaza kuwa kinapanga mikakati ya kumlazimisha Rais mkongwe wa nchi hiyo, Robert Mugabe ang'atuke madarakani baada ya kuitawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 37.
-
Kuendelea mvutano wa kisiasa nchini Zimbabwe
Nov 17, 2017 11:43Zikiwa zimepita siku kadhaa tangu yalipojiri mapinduzi baridi ya kijeshi nchini Zimbabwe, wingu la mgogoro wa kisiasa lingali limetanda ndani ya nchi hiyo huku hatima ya mgogoro wenyewe ikibaki kuwa kitendawili.
-
Mugabe kutana kwa nyuso za bashasha na wanajeshi; akataa mwito wa kujiuzulu
Nov 17, 2017 03:55Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ambaye anashikiliwa katika kizuizi cha nyumbani kwa mara nyingine tena amekataa mwito wa jeshi unaomtaka ajiuzulu.