Dec 07, 2022 13:52
Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem ametuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa "Twitter" ambapo ameipongeza Morocco kwa ushindi wa timu ya kandanda ya nchi hiyo dhidi ya Uhispania hiyo jana na kufuzu kuingia robo fainali ya mechi za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Qatar.