-
Jeshi la Sudan linasema limedhibiti tena maeneo muhimu katika jimbo la Blue Nile kutoka kwa RSF
Jun 26, 2025 12:06Jeshi la Sudan limeyadhibiti tena maeneo kadhaa katika jimbo la Blue Nile, kusini mashariki mwa nchi hiyo, yaliyokuwa yakishikiliwa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) baada ya mapambano ya jeshi la Sudan dhidi ya RSF na wapiganaji wa harakati ya SPLM-N.
-
Waislamu wa Nigeria washerehekea ushindi wa Iran dhidi ya Marekani na Israel
Jun 25, 2025 05:27Waislamu nchini Nigeria wamesherehekea ushindi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran dhidi ya Marekani na utawala haramu wa Israel baada ya vita kati ya Iran na Isreal kusitishwa baada ya kudumu kwa siku 12.
-
Zakzaky: Mashambulizi ya kigaidi ya Israel yanapasa kulaaniwa duniani kote
Jun 16, 2025 03:38Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria (IMN), Sheikh Ibrahim Zakzaky amelaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran na kuelezea hujuma hizo za utawala wa Kizayuni dhidi ya nchi huru kuwa ni kitendo cha juu zaidi cha uchokozi, kinachopaswa kulaaniwa duniani kote.
-
MSF: Unyanyasaji wa kijinsia umeongezeka mashariki mwa DRC
Jun 15, 2025 09:03Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limetangaza kuwa, vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vimeongezeka mno katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Sheikh Dalhu Abdul Mumin: Mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran ni kitendo cha ugaidi
Jun 15, 2025 08:06Imamu wa Waislamu wa Kishia wa eneo la Kaskazini mwa Ghana, Sheikh Dalhu Abdul Mumin amelaani vikali mashambulizi ya kigaidi ya Israel dhidi ya Iran na kuyataja kuwa ni "kitendo cha wazi cha kigaidi cha Israel ya Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran."
-
Nigeria yalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran
Jun 15, 2025 01:06Nigeria imelaani vikali mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran na kusema uhasama huo wa Israel utatumbukiza eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) katika hali ya taharuki.
-
Afrika Kusini yalaani mashambulizi ya kigaidi ya Israel dhidi ya Iran
Jun 14, 2025 07:20Afrika Kusini usiku wa kumkia leo Jumamosi imelaani mashambulizi ya kigaidi ya Israel dhidi ya Iran na kuhimiza kufanyika juhudi za kidiplomasia za kupunguza mivutano katika eneo la Asia Magharibi.
-
Takriban Wasudan 75,000 wamekimbia Ethiopia kutafuta usalama wao
Jun 14, 2025 07:16Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi limetangaza kuwa, takriban Wasudan 75,000 wamekimbia Ethiopia kutafuta usalama wao tangu mgogoro wa uchu wa madaraka baina ya majenerali ulipozuka nchini humo zaidi ya miwili iliyopita.
-
Waliokufa maji katika ajali za boti 2 DRC wapindukia 50
Jun 14, 2025 03:33Watu wasiopungua 52 wamethibitishwa kufariki dunia huku wengine kadhaa wakitoweka baada ya boti mbili za abiria kuzama kwenye maji ya Ziwa Tumba, magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Karibu watu 50 waaga dunia kwa mafuriko nchini Afrika Kusini
Jun 12, 2025 08:56Watu karibu 50 wakiwemo wanafunzi wa Shule, wamepoteza maisha Nchini Afrika Kusini kutokana na mafuriko makubwa yaliyosababishwa na mvua kubwa inayoendelea kwenye mkoa wa Cape Mashariki.