-
UN yalaani ukiukaji wa makubaliano ya amani Libya
Jun 10, 2025 04:08Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya (UNSMIL) umelaani ukiukaji wa mapatano ya amani katika mji mkuu, Tripoli, ambapo mapigano yalizuka mapema jana Jumatatu kati ya makundi hasimu yenye silaha wakati wa sherehe za sikukuu ya Idul Adh'ha.
-
Kenya: Mwaka mmoja baada ya maandamano ya vijana kupinga mswada wa fedha
Jun 09, 2025 22:45Kenya inaadhimisha mwaka mmoja, baada ya kuzuka kwa maandamano ya vijana maarufu kama Gen Z, kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2024, uliopendekeza nyongeza ya kodi.
-
Afisa wa Sudan: Ukraine inafanya ‘kazi chafu’ ya Wamagharibi Afrika
Jun 09, 2025 07:43Afisa mmoja wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan amesema Ukraine inatekeleza "kazi chafu" ya nchi za Magharibi kwa kuunga mkono makundi yenye silaha yanayohusika na mashambulizi ya kigaidi katika mataifa ya Afrika kama vile Libya, Somalia na Niger.
-
Mwanajeshi wa Uingereza aliyembaka mwanamke Kenya akamatwa
Jun 09, 2025 03:20Mwanajeshi wa Uingereza anayehudumu katika kambi ya mafunzo ya kijeshi nchini Kenya amekamatwa kwa tuhuma za kumbaka mwanamke.
-
Jeshi la Somalia laangamiza makamanda kadhaa wa al-Shabaab
Jun 08, 2025 23:20Makamanda watatu waandamizi wa kundi la kigaidi la al-Shabab walioendesha wimbi la mashambulizi mabaya nchini Somalia katika miezi ya karibuni wameuawa katika operesheni ya pamoja ya usalama.
-
Rwanda yajiondoa katika muungano wa Afrika ya Kati ikitoa lawama kwa DRC
Jun 08, 2025 09:01Rwanda imetangaza kujiondoa katika Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati (ECCAS), ikimshutumu nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa "kutumia njama kushawishi nadharia ya" umoja huo.
-
Wananchi wa Morocco waandamana na kuchoma moto bendera ya Israel
Jun 08, 2025 09:01Maelfu ya wananchi wa Morocco wameandamana na katika miji mbalimbali ya nchi hiyo Rabat, mji mkuu wa nchi hiyo wakilaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Gaza.
-
Wafadhili walaani mashambulizi dhidi ya raia nchini Sudan
Jun 08, 2025 02:48Nchi 30 wafadhili duniani zimelaani mashambulizi dhidi ya raia na wafanyakazi wa masuala ya kibinadamu nchini Sudan na kutaka mashambulio hayo yakomeshwe mara moja.
-
Kundi la Wagner latangaza kuondoka Mali baada ya zaidi ya miaka 3
Jun 08, 2025 02:48Kampuni binafsi ya kijeshi ya Russia maarufu kwa jina la Wagner imetangaza kuwa imeamua kuondoka nchini Mali, na hivyo kumaliza zaidi ya miaka mitatu ya operesheni zake katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
-
UN yapongeza uamuzi wa Libya wa kushughulikia masuala ya usalama
Jun 08, 2025 02:47Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya (UNSMIL) umekaribisha uamuzi wa Baraza la Uongozi la Libya wa kuunda kamati mbili za kushughulikia masuala ya usalama na haki za binadamu kufuatia mapigano ya hivi karibuni ya silaha katika mji mkuu Tripoli.