-
Zuma amkosoa Trump madai ya 'mauaji ya kimbari' Afrika Kusini, asema ni porojo tupu
Jun 04, 2025 22:45Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, amemshutumu Rais wa Marekani Donald Trump kwa kile alichokiita "porojo zisizo na msingi", baada ya Trump kudai kwamba kuna mauaji ya kimbari yanayoendelea nchini Afrika Kusini.
-
Afrika yaendelea kusukuma juhudi za kupata Kiti cha Kudumu katika Baraza la Usalama la UN
Jun 04, 2025 22:42Bara la Afrika limeendeleza msimamo wake wa kutaka uwakilishi wa kudumu ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kufuatia kikao cha 13 cha Mawaziri wa Kamati ya Umoja wa Afrika ya Nchi Kumi (C-10), kilichofanyika Jumatano hii jijini Lusaka, mji mkuu wa Zambia.
-
UNHCR: Mgogoro mpya Sudan Kusini “umeng’oa” zaidi ya watu 165,000 ndani ya miezi mitatu
Jun 04, 2025 09:43Zaidi ya watu 165,000 wamelazimika kukimbia makazi yao na kukimbilia usalama wao maeneo mengi kutokana na mivutano na migogoro ambayo inazidi kuongezeka nchini Sudan Kusini katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.
-
Wanajeshi wa Algeria waangamiza magaidi karibu na mpaka wa Tunisia
Jun 04, 2025 09:42Wizara ya Ulinzi ya Algeria imetangaza kuwa, jeshi la nchi hiyo limeangamiza magaidi wawili wenye silaha katika operesheni inayoendelea ya kukabiliana na magenge ya kigaidi katika mkoa wa mashariki wa Khenchela, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Tunisia.
-
UN: Wakimbizi milioni 4 wametoroka vita Sudan
Jun 04, 2025 02:38Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya watu milioni 4 wamekimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan.
-
Tanzania: Jamii ya kimataifa idhibiti vyanzo vya migogoro duniani
Jun 04, 2025 02:30Tanzania imeiasa jamii ya kimataifa kuweka mikakati madhubuti ikiwemo kuwashirikisha wanawake katika masuala ya amani na usalama, ili kudhibiti migogoro ambayo vyanzo vyake vikuu ni ukabila, ubaguzi wa rangi, itikadi kali na migogoro kuhusu maliasili na mipaka.
-
Watu 200 wafariki dunia kwa janga la mafuriko Nigeria
Jun 04, 2025 02:21Mafuriko makubwa yaliyotokea kaskazini mwa Nigeria wiki iliyopita yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 200.
-
Serikali ya Sudan yalituhumu kundi la RSF kwa kulenga msafara wa misaada Darfur
Jun 03, 2025 23:22Serikali ya Sudan imetangaza kwamba "Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vililenga msafara wa misaada wa Umoja wa Mataifa katika eneo la Al-Koma katika jimbo la Darfur Kaskazini."
-
Niger yazituhumu nchi za Magharibi kwa njama za kuvuruga utawala wake
Jun 03, 2025 23:16Rais wa mpito wa Niger, Jenerali Abdourahamane Tchiani, amezituhumu nchi za Magharibi, hasa Ufaransa, kwa kuchochea machafuko ya kigaidi nchini humo kama njia ya kujaribu kulazimisha “mfumo mpya wa utawala” kinyume na matakwa ya raia wa Niger.
-
HRW: Waasi wa M23 waliwaua raia mashariki mwa DRC mwezi Februari
Jun 03, 2025 23:02Shirika moja kimataifa la kutetea haki za binadamu, limeripoti kuwa waasi wa M23 waliwaua kwa makusudi raia wasiopungua 21 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) mwezi Februari mwaka huu.