-
Hamas yasifu msimamo wa viongozi wa Afrika dhidi ya Israel
Feb 18, 2025 01:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina , Hamas, imesifu msimamo wa "kiadilifu na jasiri" wa viongozi wa Afrika kuhusu mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza, pamoja na upinzani wao mkali dhidi ya kampeni ya kikatili inayoendelea dhidi ya Wapalestina.
-
UN na washirika wake wazindua ombi la dola bilioni sita kusaidia watu milioni 26 Sudan
Feb 18, 2025 01:02UN na washirika wake wamezindua ombi la dola bilioni sita kusaidia watu milioni 26 Sudan
-
Serikali ya DRC yasema Jeshi la Rwanda limeingia Bukavu Mashariki
Feb 18, 2025 00:58Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imesema kuwa jeshi la Rwanda na washirika wake wameingia katika mji wa Bukavu, mashariki mwa nchi hiyo, katika jimbo la Kivu Kusini, na kuwataka wananchi kuwa macho.
-
Maelfu ya Wakongo kutoka mashariki mwa nchi wakimbilia Burundi
Feb 17, 2025 07:56Maelfu ya raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamekimbilia katika nchi jirani ya Burundi wakikimbia machafuko katika maeneo yao.
-
AU yataka Israel ishtakiwe kwa mauaji ya kimbari ya Ghaza na kutoshirikiana wala kuanzisha uhusiano nayo
Feb 17, 2025 03:39Wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika AU wametoa wito, mwishoni mwa mkutano wa 38 wa kilele uliofanyika mjini Addis Ababa, wa kusitishwa ushirikiano na kutoanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Maonyesho ya "Qur'ani katika Macho ya Wengine" yafunguliwa Tunisia
Feb 17, 2025 01:04Maonyesho ya "Qur'ani katika Macho ya Wengine" yamefunguliwa katika Maktaba ya Kitaifa ya Tunisia, na yataendelea hadi Aprili 30, kwa ushirikiano wa Taasisi ya Urithi wa Kitaifa na Taasisi ya Utafiti wa Kisasa wa Maghreb.
-
Waziri Mkuu wa zamani wa Mauritius akamatwa kwa tuhuma za utakatishaji pesa
Feb 16, 2025 23:37Waziri Mkuu wa zamani wa Mauritius Pravind Jugnauth amekamatwa na anakabiliwa na shtaka la utakatishaji pesa. Hayo yameelezwa na Tume ya Uhalifu wa Kifedha inayoendeshwa na serikali ya nchi hiyo.
-
Kumalizika mkutano wa 38 wa wakuu Umoja wa Afrika Addis Ababa
Feb 16, 2025 23:04Mkutano wa 38 wakuu wa Umoja wa Afrika ulimalizika jana katika makao makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa Ethiopia.
-
Katibu Mkuu wa UN aahidi Afrika kuwa na mwakilishi wa kudumu kwenye Baraza la Usalama
Feb 16, 2025 10:43Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema sio sawa kwa bara la Afrika kutokuwa na kiti cha mwakilishi wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na ameahidi kufanya kazi na Umoja wa Afrika na nchi wanachama ili kuhakikisha kuwa nchi za Afrika zinapata mwakilishi wa kudumu katika Baraza la Usalama.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini: Tunapinga kufurushwa Wapalestina, hatutasalimu amri mbele ya vitisho vya Trump
Feb 16, 2025 10:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Ronald Lamola, amesema kuwa nchi za bara hilo zina msimamo mmoja juu ya haja ya kusuluhisha mgogoro wa Ukanda wa Gaza ndani ya suluhisho la mataifa mawili, akisisitiza kwamba Pretoria haitarudi nyuma kuhusiana na msimamo wake katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki.