-
67 wauawa katika shambulizi la wanamgambo kwenye mji wa El Fasher, magharibi mwa Sudan
Feb 03, 2025 23:15Jeshi la Sudan SAF limetangaza kuwa, takriban watu 67 waliuawa Jumapili katika shambulizi la mizinga lililofanywa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) huko El Fasher, makao makuu ya Jimbo la Darfur Kaskazini la magharibi mwa Sudan.
-
Ramaphosa apinga bwabwaja mpya za rais wa Marekani, asema hakuna ardhi iliyotwaliwa na Afrika Kusini
Feb 03, 2025 06:59Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini leo Jumatatu amepinga bwabwaja na madai ya rais wa Marekani Donald Trump na kusema kuwa Pretoria haijawahi kunyang'anya ardhi yoyote ile.
-
Watu 54 wauawa na 158 wajeruhiwa katika shambulio la kijeshi sokoni huko Omdurman nchini Sudan
Feb 03, 2025 06:58Idadi ya watu waliouawa kutokana na kushambuliwa kwa makombora na wapiganaji wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) siku ya Jumamosi kwenye soko lenye watu wengi huko Omdurman, kaskazini mwa mji mkuu wa Sudan Khartoum, imeongezeka na kukfikia 54.
-
Jeshi la Tanzania lathibitisha kuuwa askari wake wawili DRC, Rwanda yakaribisha kujadiliwa mzozo
Feb 03, 2025 02:23Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetangaza kuwa, wanajeshi wake wawili ni miongoni mwa askari 20 wa kulinda amani waliouawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Burundi yaonya kuhusu kutokea vita vikubwa vya kikanda
Feb 02, 2025 23:56Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye ameonya kuwa mzozo unaoongezeka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unaweza kuzusha vita vikubwa zaidi vya kikanda katika eneo la Maziwa Makuu.
-
DRC yataka Arsenal, Bayern Munich na PSG kufuta kandarasi zao na Rwanda
Feb 02, 2025 22:56Mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Rwanda umeingia katika hatua mpya baada ya Kinshasa kuvitaka vilabu vya soka barani Ulaya vyenye kandarasi na serikali ya Kigali kusitisha kandarasi hizo.
-
Museveni apuuza uamuzi wa mahakama juu ya mahakama za kijeshi
Feb 02, 2025 09:00Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amesema serikali yake itaendelea kuwashtaki raia katika mahakama za kijeshi, licha ya Mahakama ya Juu ya nchi hiyo kupiga marufuku hatua hiyo, ikisema ni kinyume cha katiba.
-
Utulivu wa kulegalega washuhudiwa Goma; Mapigano yapungua mashariki mwa DRC
Feb 02, 2025 04:15Ripoti mbalimbali zinaeleza kuwa licha ya kurejea utulivu wa kiwango fulani katika mji wa Goma, makao makuu ya jimbo la Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mashirika ya misaada ya kibinadamu yameonya juu ya kushtadi hali ya mambo huku hospitali zikizidiwa na wagonjwa, uhaba wa vifaa muhimu vya tiba ukishuhudiwa na miili ya watu waliouawa ikiendelea kuonekana mitaani.
-
Takriban watu 56 wameuawa Sudan huku mapigano yakiendelea Khartoum
Feb 02, 2025 04:07Mashambulio ya mizinga na ya anga yalisababisha vifo vya takriban watu 56 jana Jumamosi katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum. Haya yameelezwa na duru za hospitali na wanaharakati wa Sudan.
-
Zaidi ya watu milioni 67 wana uhaba wa chakula Pembe ya Afrika
Feb 01, 2025 23:21Takriban watu milioni 67.4 wa eneo la Pembe ya Afrika hawana uhakika wa chakula. Hayo yametangazwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali ya Afrika Mashariki (IGAD).