-
Kundi la Mgogoro: Uasi huko Goma, DRC, Unaweza Kusababisha Vita vya Kikanda
Jan 30, 2025 23:23Kundi la International Crisis Group limesema kuwa waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameuvamia mji wa Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuudhibiti mji huo wenye watu milioni moja.
-
Vyanzo vya jeshi Sudan: Dagalo anatekeleza Mpango B katika vita vya ndani
Jan 30, 2025 23:19Vyanzo vya kijeshi katika Wizara ya Ulinzi ya Sudan vimefichua kwamba Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) hivi sasa vinatekeleza Mpango B (mpango mbadala) ambao kamanda wake, Mohamed Hamdan Dagalo "Hemedti", alitishia kuutekeleza baada ya kushindwa kunyakua madaraka.
-
Binti wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Zuma akamatwa kwa tuhuma za ugaidi
Jan 30, 2025 10:29Binti wa aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, amekamatwa na alitarajiwa kufikishwa mahakamani leo Alhamisi kujibu mashtaka ya ugaidi.
-
Rais Tshisekedi aapa kuendesha vita 'vikali' vya kuwakomesha waasi wa M23
Jan 30, 2025 08:45Rais Félix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ameapa kurejesha mamlaka ya serikali mashariki mwa nchi, ambako waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameuteka mji wa Goma na wanaripotiwa kuelekea kusini kuchukua maeneo zaidi.
-
UN: Hali ya Goma DRC imetulia, kuna ufyatuaji risasi na uporaji wa hapa na pale
Jan 30, 2025 02:20Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kwamba, hali katika mji wa Goma wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ni shwari lakini bado ni ya wasiwasi, huku baadhi ya vurugu zikikwamisha shughuli za kibinadamu.
-
Libya yakomboa wahamiaji 263 waliokuwa wanashikiliwa na wahalifu wanaotaka kikomboleo
Jan 30, 2025 02:19Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Libya imetangaza habari ya kukombolewa wahamiaji 263 waliokuwa wametekwa na genge la wahalifu katika mji wa mashariki wa Jalu kwa ajili ya kupata kikomboleo.
-
Rais wa Sudan Kusini atoa amri ya kufanyika uchunguzi wa ajali ya ndege iliyoua watu 20
Jan 30, 2025 02:19Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini ameamuru uchunguzi ufanyike kuhusu ajali ya ndege iliyotokea jana Jumatano asubuhi na kusababisha vifo vya watu 20 wakiwemo raia wa kigeni katika Jimbo la Unity.
-
Wafadhili waahidi dola bilioni 8 kusambaza umeme Afrika
Jan 29, 2025 22:27Benki ya Maendeleo ya Afrika na wakopeshaji wengine wa kimataifa wameahidi zaidi ya dola bilioni 8 zitakazotumika kwenye mkakati wa kuwawezesha Waafrika milioni 300 kupata umeme katika kipindi cha miaka sita ijayo. Mpango huo unaoitwa "Mission 300" uliozinduliwa na Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika mwezi Aprili, unakadiriwa kugharimu dola bilioni 90.
-
Niger, Mali na Burkina Faso zajiondoa rasmi ECOWAS
Jan 29, 2025 22:25Serikali za kijeshi za Niger, Mali na Burkina Faso zimejiondoa rasmi kwenye Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS).
-
Waasi wa M23 wakaribia kudhibiti kikamilifu mji muhimu wa Goma DRC
Jan 29, 2025 09:16Waasi wa M23 wanaonekana kukaribia kuudhibiti mji muhimu wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia ripoti kwamba wameuteka uwanja wake wa ndege.