-
Maharusi 1,000 kutoka mataifa 43 ya Afrika wajumuika pamoja nchini Ethiopia
Jan 27, 2025 23:27Zaidi ya maharusi na wanandoa 1,000 kutoka mataifa 43 tofauti ya Afrika walijumuika pamoja Jumapili kushiriki katika sherehe ya harusi ya kiutamaduni na hilo ni tukio la kwanza la aina yake katika kipindi cha miaka kumi iliyopita.
-
Ruto: Afrika inapoteza dola bilioni 18 kila mwaka kutokana na mizozo
Jan 27, 2025 23:26Rais William Ruto wa Kenya ambaye yuko mstari wa mbele katika kupigania mageuzi ya kitaasisi ndani ya Umoja wa Afrika (AU), alisema jana Jumatatu kwamba mizozo inaendelea kuinyima Afrika uwezo wake na inalitia hasara kubwa bara hilo. Hasara hiyo inakadiriwa kufikia dola bilioni 18 kila mwaka na kuwafanya mamilioni ya Waafrika kuwa wakimbizi.
-
Wahamiaji 1,313 waliokolewa katika pwani ya Libya wiki iliyopita
Jan 27, 2025 23:25Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema kwenye taarifa yake ya jana Jumatatu kuwa wahamiaji 1,313 waliokolewa kwenye pwani ya Libya wiki iliyopita.
-
Interpol yawakamata magaidi 37 Afrika Mashariki
Jan 27, 2025 08:59Polisi ya Kimataifa (Interpol) imesema washukiwa 37 wa ugaidi, wakiwemo kadhaa wanaoaminika kuwa wanachama wa ISIS, wamekamatwa katika kanda ya Afrika Mashariki katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.
-
Jeshi la Nigeria laangamiza magaidi 70 wa Boko Haram
Jan 27, 2025 08:55Wizara ya Ulinzi ya Nigeria imesema wanamgambo wasiopungua 70 wa Boko Haram waliuawa katika msururu wa operesheni za karibuni za kijeshi katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Mkuu wa MONUSCO awataka waasi wa M23 kuondoka Kongo
Jan 27, 2025 04:37Mkuu wa kikosi cha wanajeshi wa kulinda amani cha Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO) amewataka waasi wa kundi la M23 kusitisha harakati zao na kuondoka nchini humo.
-
Human Rights Watch: Mzozo DRC unaweza kuleta maafa ya kibinadamu
Jan 26, 2025 23:15Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limetahadharisha kuhusiana na mapigano yanayoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kueleza uwezekano wa kutokea maafaa ya kibinadamu.
-
Makumi ya wanajeshi wa Nigeria wauawa katika shambulio la kigaidi
Jan 26, 2025 22:55Watu wanaoshukiwa kuwa magaidi wamewaua wanajeshi 20 wa Nigeria, akiwemo kkamanda wa ngazi ya juu, baada ya kushambulia kambi moja ya jeshi katika jimbo la Borno la kaskazini mashariki.
-
Askari wa kulinda amani waliouawa DRC waongezeka na kufikia 13, mapigano yazidi kupamba moto
Jan 26, 2025 08:05Idadi ya askari wa kulinda amani waliouawa katika mapigano na waasi wa M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC imefikia 13.
-
Jeshi la Sudan ladhibiti kikamilifu kiwanda kikubwa zaidi cha kusafisha mafuta nchini humo
Jan 26, 2025 03:24Jeshi la Sudan limeeleza kuwa limechukua udhibiti kamili wa kiwanda cha kusafisha mafuta cha al Jaili karibu na mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum huku gavana mmoja wa nchi hiyo akiripoti kuuawa watu zaidi ya 70 katika shambulio la droni lililotekelezwa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) huko al Fasher magharibi mwa Sudan.