-
Uganda: Serikali yazima mtandao wa intaneti siku moja kabla ya uchaguzi mkuu
Jan 14, 2026 07:24Serikali ya Uganda imezima mtandao wa intaneti siku moja kabla ya kuelekea uchaguzi mkuu wa hapo kesho, uchaguzi ambao Rais Yoweri Museveni anataka kuchaguliwa kwa muhula wa saba.
-
Afrika yakosoa hatua ya Trump ya kuiondoa US katika taasisi za kimataifa
Jan 14, 2026 03:15Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Mahmoud Ali Youssouf ametoa wito wa kuimarishwa mifumo ya pande nyingi ili kushughulikia changamoto za kimataifa, siku chache baada ya Marekani kuchukua uamuzi wa upande mmoja wa kujiondoa katika taasisi mbalimbali za kimataifa.
-
Jeshi la Somalia laangamiza magaidi 17 wa al-Shabaab
Jan 14, 2026 02:56Wizara ya Ulinzi wa Somalia imesema kwamba, Jeshi la Kitaifa la nchi hiyo limewaua magaidi 17 wa al-Shabaab katika operesheni ya anga iliiyofanyika kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Misri 'yakaribisha' kuwekwa Ikhwani katika orodha ya magaidi ya US
Jan 14, 2026 02:52Serikali ya Misri imepongeza hatua ya Marekani ya kuitambua rasmi Harakati ya Kiislamu ya Ikhwanul Muslimin kuwa ni shirika la kigaidi.
-
Maporomoko ya udongo mashariki mwa Kongo yauwa takriban watu 13
Jan 13, 2026 23:37Takriban watu 13 wamepoteza maisha kufuatia maporomoko ya udongo yaliyotokea mashariki mwa Kongo mapema jana Jumanne. Watu wengien zaidi ya 30 hawajulikani waliko hadi sasa.
-
Uganda yaamuru mashirika ya haki kusitisha shughuli zao
Jan 13, 2026 23:10Uganda imeamuru mashirika mawili ya haki kusitisha shughuli zao, siku moja kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu ambao Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeutaja kuwa unafanyika katika mazingira ya ukandamizaji na vitisho.
-
Somalia yaitaka Israel kubatilisha mara moja uamuzi wake wa kuitambua Somaliland
Jan 13, 2026 23:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Somalia ameitaja hatua ya utawala ghasibu wa Israel ya kulitambua eneo la Somaliland kuwa ni ukiukaji wa wazi wa mamlaka ya nchi yake.
-
Somalia yafuta mikataba yote iliyosainiwa na UAE
Jan 13, 2026 02:33Somalia imeamua kufuta makubaliano yote yaliyosainiwa na Umoja wa Falme za Kiarabu, ili kukabiliana na hatua za Abu Dhabi zinazodhoofisha mamlaka, umoja na uhuru wa nchi hiyo. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Baraza la Mawaziri la Somalia.
-
RSF yaua watu 27 huko Sennar, mashariki mwa Sudan
Jan 13, 2026 02:10Watu 27 wameuawa na wengine 13 kujeruhiwa katika shambulio la wapiganaji wa Rapid Support Forces lililolenga mji wa Sinja, wakati watu waliokimbia makazi yao kutoka Darfur Kaskazini wakiendelea kuongezeka, huku Jeshi la Sudan likitangaza mauaji ya mamia ya wanachama wa RSF katika maeneo tofauti.
-
Ghana imelipa deni la dola bilioni 1.47 la sekta ya nishati
Jan 13, 2026 00:13Ghana imelipa jumla ya dola za Marekani bilioni 1.47 mwaka 2025 ili kufuta madeni ya muda mrefu ya sekta ya nishati na kurejesha dhamana ya Benki ya Dunia kwa sekta hiyo. HIi ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Jumatatu na Wizara ya Fedha ya nchi hiyo.