-
Viongozi wa Kiafrika wahimizwa kudumisha 'ujasiri' katika kushinikiza fidia ya utumwa
Dec 20, 2025 10:40Rais wa Ghana, John Dramani Mahama, amekutana na kuzungumza wajumbe wa kimataifa, lengo likiwa ni kutafuta fidia ya utumwa na ukoloni wa Wazungu katika maeneo mbalimbali ya dunia hasa barani Afrika.
-
Wanamgambo wa RSF wamewaachia huru wafanyakazi 9 wa sekta ya afya huko Darfur
Dec 20, 2025 10:33Mtandao wa Madktari nchini Sudan umeripoti kuwa wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) umewaachia huru wafanyakazi 9 wa sekta ya afya waliokuwa wakishikiliwa katika magareza na kikosi hicho huko Nyala makao makuu ya jimbo la Darfur Kusini. Hata hivyo kikosi cha RSF bado kinawashikilia wafanyakazi wengine wa afya 73.
-
Muda wa kuhudumu askari wa UN nchini DRC waongezwa huku waasi wakishadidisha vita
Dec 20, 2025 03:43Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kauli moja jana Desemba 19, 2025 limepitisha azimio namba 2808 (2025), ambalo linaamua kuongeza hadi tarehe 20 Desemba 2026 muda wa kazi wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (MONUSCO), na kwa hali ya kipekee, wa brigedi yake ya kukabiliana mashambulizi.
-
Rais Museveni: Tuna risasi za kutosha kukabiliana na wanaopanga kuandamana
Dec 20, 2025 00:33Rais Yoweri Museveni wa Uganda amewaonya wale wanaopanga kuandamana na kueleza kwamba, kuna risasi za kutosha kwa ajili ya kukabiliana nao.
-
Mashambulizi ya RSF yaua raia 16 eneo la Kordofan, Sudan
Dec 19, 2025 23:07Takriban watu 16 wameuawa katika shambulio la mizinga la waasi wa RSF lililolenga mji uliozingirwa katika eneo la Kordofan nchini Sudan, huku vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo vikiingia katika awamu hasasi kwenye mwaka wake wa tatu.
-
Mauaji yaongezeka Western Cape hasa Cape Town, nchini Afrika Kusini
Dec 19, 2025 07:19Takwimu za hivi karibuni zaidi za vitendo vya uhalifu nchini Afrika Kusini zinaonesha kuwa zaidi ya watu 1,000 waliuawa katika Mkoa wa Western Cape kati ya mwezi Julai na Septemba mwaka huu, huku Cape Town ikiwa kitovu cha vitendo vya uhalifu na vurugu katika eneo hil.
-
Mvurugiko wa hali ya hewa, Morocco yakumbwa na mawimbi ya baridi kali
Dec 19, 2025 07:18Katika kile kinachoonekana wazi kuwa ni madhara ya uchafuzi wa mazingira na mvurugiko wa hali ya hewa kutokana na uharibifu mkubwa wa hewa unaofanywa na madola ya viwanda duniani, taarifa kutoka Morocco zinasema kuwa, nchi hiyo ya jangwa imekumbwa na mawimbi makubwa ya baridi kali ambayo hayajawahi kutokea.
-
Rais wa Zambia aidhinisha sheria ya kupanua Bunge miezi kadhaa kabla ya uchaguzi
Dec 19, 2025 03:15Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema, jana Alkhamisi alisaini sheria ambayo itapanua Bunge la nchi hiyo, hatua ambayo wakosoaji wanasema inaweza kukinufaisha chama chake, miezi minane kabla ya uchaguzi wa kitaifa.
-
Jenerali Mkuu wa Sudan akutana na Rais wa Misri, vita vinaendelea
Dec 19, 2025 07:19Jenerali Mkuu wa Sudan, Abdel-Fattah al Burhan, amekutana na Rais wa Misri, Abdel-Fattah el-Sissi mjini Cairo huku kukiwa na shinikizo linalozidi kuongezeka la kuhimiza kutatuliwa mgogoro wa vita nchini Sudan haraka iwezekanavyo.
-
UN: Zaidi ya raia 1,000 waliuawa katika shambulio la RSF Darfur
Dec 18, 2025 08:22Ripoti iliyotolewa Alkhamisi na Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema zaidi ya raia 1,000 waliuawa wakati kundi la waasi wa Sudan lilipotwaa udhibiti wa kambi ya wakimbizi wa ndani huko Darfur nchini Sudan mwezi Aprili mwaka huu.