-
Waziri wa zamani Kenya: Rais Ruto anawalazimisha mawaziri kufanya anachotaka kwa woga
Jul 31, 2026 10:04Waziri wa zamani wa Fedha wa Kenya, Prof Njuguna Ndung’u, amemshutumu Rais wa nchi hiyo, William Ruto kwa kuingilia utendakazi wa taasisi huru, akisema mtindo huu umezorotesha uwezo wa kutekeleza majukumu ipasavyo.
-
Watu kadhaa wafa maji, mamia ya Wamorocco wakimbilia Ceuta ya Uhispania
Jul 31, 2026 08:37Wimbi la wahamiaji kutoka Morocco kuelekea mji unaodhibitiwa na Uhispania wa Ceuta limegeuka kuwa mgogoro wa kibinadamu na kisiasa, baada ya miili ya wahamiaji tisa kuopolewa majini. Wahamiaji hao waliaga dunia wakiwa katika jitihada za kuogelea hadi mjini huo.
-
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye, amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi
Jul 30, 2026 14:53Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye, amelazwa hospitalini na hana fahamu baada ya kuziraia akiwa mahakamani jana Jumatano. Hayo ni kwa mujibu wa mkewe na watu wengine wanaozihimiza mamlaka husika nchini Uganda kumwachilia huru baada ya kunyimwa dhamana mara kwa mara.
-
Upinzani DRC wakasirika baada ya Mahakama kumfungulia njia rais Tshisekedi kugombea muhula wa tatu
Jul 30, 2026 10:19Wanasiasa wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, ambao ni wanachama wa muungano wa upinzani uliopewa jina la utani "C64", wamepinga vikali uamuzi wa Mahakama ya Katiba kuhusu sheria ya kura ya maoni, ambayo inaweza kumfungulia njia Rais wa nchi hiyo Felix Tshisekedi kugombea urais kwa muhula wa tatu baada ya kura hiyo ya maoni.
-
WHO yaonya kuwa Uganda ingali iko katika hatari ya mripuko wa ebola
Jul 30, 2026 10:15Shirika la Afya Duniani, WHO leo limetoa indhari kwa Uganda kwamba ingali iko katika hatari kutokana na mripuko wa ugonjwa wa Ebola ulioenea katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Rais wa Algeria akemea ‘serikali ndogo’ ya kikanda kwa uvurugaji usalama, akusudia UAE
Jul 29, 2026 14:19Rais wa Algeria, Abdelmadjid Tebboune, ameikosoa vikali “serikali ndogo” ya kikanda ambayo hakuitaja jina, lakini inafahamika wazi kuwa alikusudia Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), kutokana na mchango wake wa kuvuruga usalama na utulivu katika ulimwengu wa Kiarabu na ukanda wa Sahel eneo la Afrika Magharibi, akionya kuwa Algeria itasimama imara kulinda mamlaka yake.
-
Uganda yatangaza kumalizika kwa mlipuko wa homa ya Ebola nchini humo
Jul 29, 2026 14:16Mamlaka nchini Uganda zimetangaza kuwa nchi hiyo sasa haina maambukizi ya virusi vya Ebola, huku maambukizi ya ugonjwa huo wa homa ya kutokwa damu yakiendelea kuongezeka katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
-
Al-Burhan atembelea miji ya kimkakati ya Sudan iliyokombolewa kutoka kwa RSF
Jul 29, 2026 02:19Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan ametembelea miji ya Umm Sayala na Jabrat al-Sheikh katika jimbo la Kordofan Kaskazini siku moja baada ya jeshi kuchukua udhibiti wa maeneo mawili kutoka kwa wapiganaji wa RSF.
-
Watu wenye silaha waua raia wasiopungua 30 jimboni Kaduna, Nigeria
Jul 28, 2026 14:02Watu wasiopungua 30 wameuawa wakati genge la wenye silaha liliposhambulia kijiji kimoja katika jimbo la Kaduna kaskazini magharibi mwa Nigeria. Hayo yamethibitishwa na wakazi wawili wa kijiji hicho.
-
Chad kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, yasema inaziandama zaidi nchi za Afrika
Jul 28, 2026 03:52Chad imejiunga na orodha inayoongezeka ya nchi zilizoanza taratibu za kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ikisema inaziandama zaidi nchi za Afrika.