-
Matokeo ya uchaguzi wa rais wa Cameroon kutangazwa Jumatatu
Oct 23, 2025 23:25Baraza la Katiba la Cameroon linasema kuwa litatangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa rais siku ya Jumatatu tarehe 27 Oktoba, saa 11 asubuhi kwa saa za huko.
-
Je, kujenga vinu vya nyuklia kutaiwezesha Afrika au kutaimarisha utegemezi wa kigeni?
Oct 23, 2025 07:44Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed mwezi uliopita alitangaza mipango ya kujenga vinu vya kwanza vya nyuklia nchini humo na hivyo kuashiria hamu kubwa ya bara la Afrika ya kumiliki nishati ya atomiki. Nchi za bara la Afrika zinahitaji kukidhi mahitaji ya nishati yanayoongezeka kila siku na kupunguza utegemezi wa nishati ya kisukuku.
-
Wanamgambo wa RSF waushambulia Uwanja wa Ndege wa Khartoum kwa siku ya tatu mtawalia
Oct 23, 2025 07:32Wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) leo wamefanya wimbi la mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) katika Uwanja wa Ndege wa Khartoum kwa siku ya tatu mtawalia.
-
Jiji la Nairobi katika hatari ya kusombwa na mafuriko
Oct 23, 2025 02:49Idara ya Utabiri wa Hali ya Hewa nchini Kenya imetoa onyo la mvua kubwa, katika maeneo kadhaa ya nchi, huku jiji la Nairobi likitajwa kuwa miongoni mwa maeneo yaliyo katika hatari kubwa ya kusombwa na mafuriko.
-
Wahamiaji karibu 40 wapoteza maisha baada ya boti kupinduka katika pwani ya Tunisia
Oct 23, 2025 02:15Afisa mmoja wa serikali ya Tunisia amesema kuwa takriban wahamiaji 40 kutoka Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara wamefariki dunia baada ya mashua yao kupinduka katika pwani ya Tunisia jana Jumatano, katika mojawapo ya ajali mbaya zaidi za meli katika eneo hilo katika mwaka huu.
-
Makumi waaga dunia katika mlipuko wa lori la mafuta nchini Nigeria
Oct 22, 2025 23:03Makumi ya watu wameripotiwa kufariki dunia katika mlipuko wa lori la mafuta nchini Nigeria. Ripoti zinasema tukio hilo limetokea katika jimbo la kati la Niger nchini Nigeria baada ya gari hilo kuteleza kutoka barabarani na kuanguka, na kumwaga mafuta.
-
Watu 46 wamefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani Uganda
Oct 22, 2025 09:27Polisi ya Uganda imeripoti kuwa watu 46 wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha mabasi mawili katika barabara kuu ya Kampala kuelekea Gulu nchini humo mapema leo Jumatano.
-
DR Congo yaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi wanaoshambulia kambi zake za kijeshi
Oct 22, 2025 02:45Wanajeshi wawili wa Rwanda wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kuwaunga mkono waasi wa Machi 23 (M23) waliofanya mashambulizi mapema juzi Jumatatu dhidi ya kambi za kijeshi za serikali huko kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
-
IOM: Licha hali ya tete ya usalama, zaidi ya watu milioni moja wamerejea mji mkuu wa Sudan, Khartoum
Oct 21, 2025 23:48Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetangaza kuwa, watu zaidi ya milioni moja wamerejea katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, katika kipindi cha miezi 10 iliyopita licha ya kukosekana usalama wa kutosha katika mji huo kutokana na vita vinavyoendelea nchini humo.
-
Ethiopia ambayo ni mwanachama wa BRICS yaanza mchakato wa kubadili deni la dola kuwa Yuan
Oct 21, 2025 08:58Ethiopia imeanza mazungumzo na China kuhusu kubadili sehemu ya deni lake la dola bilioni 5.38 kuwa mikopo inayotumia sarafu ya yuan, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kupunguza shinikizo la fedha za kigeni na kuimarisha uhusiano wa kibiashara.