-
Mamia waandamana Uvira, Congo DR, wanataka Jenerali Gasita aondolewe madarakani
Sep 08, 2025 23:43Mamia ya wakazi wa Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, waliandamana jana Jumatatu katika mitaa ya mji huo dhidi ya serikali wakiitikia wito wa mashirika ya kiraia.
-
Wakenya 66,000 kupoteza ajira ikiwa makubaliano ya AGOA hayatatazamwa upya
Sep 08, 2025 08:52Sheria ya Ukuaji na Fursa Barani Afrika (AGOA) inatazamiwa kumalizika muda wake ifikapo tarehe 30 mwezi huu wa Septemba, na hivyo kuhitimisha mpango muhimu wa biashara bila ushuru kati ya Kenya na Marekani.
-
Familia ya Rais wa zamani wa Zambia katika mazungumzo ya upatanishi kumaliza mzozo wa mazishi
Sep 08, 2025 08:46Nchini Zambia, kuna uwezekano wa kufikiwa mwafaka kuhusu mazishi ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Edgar Lungu wakati serikali na familia yake zikianza mazungumzo ya upatanishi ili kutatua mzozo wa muda mrefu kuhusu taratibu ya mazishi ya mwanasiasa huyo.
-
Waasi wa M23 wauteka tena mji wa Shoa katika jimbo la Kivu kaskazini
Sep 08, 2025 04:02Waasi wa kundi la M23 jana waliuteka tena mji wa Shoa katika jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya mapigano na wanajeshi wanaoiunga mkono serikali ya Kinshasa.
-
Shirika la Uhamiaji la Somalia na jitihada za kupambana na misimamo mikali
Sep 08, 2025 04:02Shirika la Uhamiaji la Somalia linafanya kazi kwa bidii kupambana na vitendo vya uchupaji mipaka na misimamo mikali na kuimarisha usalama katika mipaka ya nchi hiyo kwa kushirikiana na washirika wa kimataifa.
-
DRC: Maelfu ya wanafunzi wa Kivu washindwa kurudi shule kutokana na mapigano
Sep 07, 2025 23:02Maelfu ya wanafunzi wa Kivu Kusini na Kaskazini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameshindwa kurudi shule kutokana na mapigano yanayoendelea katika majimbo hayo.
-
WHO: Njaa imeathiri baadhi ya maeneo ya Sudan
Sep 07, 2025 08:29Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Dunuani Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema katika ujumbe wake kwenye mtandao wa kijamii wa X kwamba "Sudan inakabiliwa na mgogoro wa uhaba wa chakula na njaa katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo," akieleza kuwa hali ni mbaya haswa katika eneo la Darfur Kaskazini, ambako mji wa El Fasher unazingirwa kwa zaidi ya siku 500.
-
Boko Haram yaua zaidi ya watu 60 kaskazini mashariki mwa Nigeria
Sep 07, 2025 03:07Kundi la wapiganaji wanaoaminikka kuwa wa Boko Haram limewaua zaidi ya watu 60 katika shambulio la usiku kwenye jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Familia za waliouawa katika maandamano ya Gen Z huko Kenya zataka fidia ya 'kubadilisha maisha"
Sep 07, 2025 02:47Familia na jamaa wa Wakenya waliouawa katika maandamano ya vijana maarufu kama Gen Z, waliokuwa wakipinga Muswada wa Fedha wa mwaka 2024, uliopendekeza nyongeza ya kodi, wameiambia timu ya wataalamu walioteuliwa kushughulikia fidia kwa waathiriwa wa maandamano hayo kuwa wanataka kulipwa fidia itakayobadili maisha yao.
-
Mjukuu wa Mandela: Hatutawaacha Wapalestina peke yao
Sep 06, 2025 22:55Mjukuu wa kiongozi wa mapambano ya ukombozi wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela, Mandla Mandela amesisitiza kuwa, kamwe hatutawaacha peke yao Wapalestina huko Gaza na maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na Israel.