-
Waziri wa Mambo ya Nje: Iran itajibu barua ya Trump
Mar 20, 2025 23:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kwamba Jamhuri ya Kiislamu itajibu barua ya Rais wa Marekani Donald Trump katika siku zijazo kupitia njia zinazofaa.
-
Salamu za Nouruzi za Rais Pezeshkian kwa Wairan: Tutaifanya qadar yetu iwe bora na tukufu zaidi
Mar 20, 2025 09:18Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza katika ujumbe na salamu zake za Nouruzi kwa wananchi wa Iran kwamba, Nouruzi na Usiku wa Qadar (Lailatul-Qadr) ni miale miwili ya nuru moja na madhihirisho mawili ya hakika na ukweli mmoja, na akafafanua kwa kusema: "katika mzunguko mpya wa masiku, tutaifanya qadari yetu iwe bora na tukufu zaidi kuliko ilivyo sasa".
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mwaka 1404 ni "Mwaka wa Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji"
Mar 20, 2025 07:42Ayatullah Khamenei Kiongozi Muadhamu uwa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma ujumbe kwa mnasaba wa kuanza mwaka mpya wa 1404 hijria shamsia na kuutaja mwaka huu mpya kuwa ni "Mwaka wa Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji."
-
Baqaei alaani hujuma za kijeshi dhidi ya Yemen na mauaji ya kimbari Ukanda wa Gaza
Mar 20, 2025 07:04Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani kuendelea mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen na mauaji ya utawala wa Kizayuni dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
-
Mkesha wa kwanza wa Laylatul Qadr waadhimishwa Iran na maeneo mengine duniani
Mar 20, 2025 03:14Usiku wa kuamkia leo Alkhamisi yaani mwezi 19 Ramadhani, ulikuwa ni mkesha wa kwanza wa Laylatul Qadr na umeadhimishwa katika kona zote za Iran na maeneo mengine duniani.
-
Baghaei: Machi 19 ni uthibitisho wa dhamira ya Wairani ya kupinga uonevu
Mar 19, 2025 23:42Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa tarehe 29 Isfand (Machi 19), ambayo ni maadhimisho ya siku ya kufanywa mafuta ya Iran kuwa ni mali ya taifa, ni ushahidi wa azma ya kweli ya wananchi wa Iran ya kupinga uonevu.
-
Onyo la Iran kwa Marekani kuhusu matokeo mabaya ya uchokozi wa aina yoyote
Mar 19, 2025 23:04Amir Saeed Irvani, Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa alitahadharisha katika barua yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatatu kwamba, hatua zozote za kichokozi zitakazofanywa na Marekani zitakuwa na matokeo mabaya na hatari mno.
-
Iran imeuza madini yenye thamani ya dola bilioni 12 katika kipindi cha mwaka mmoja
Mar 19, 2025 08:42Mauzo ya nje ya madini ya Iran yameongezeka katika miezi 11 ya mwaka wa Kiirani hadi mwishoni mwa Februari, yakifikia jumla ya dola bilioni 12.599.
-
Masharti ya Iran katika kufanya mazungumzo na nchi za Magharibi
Mar 19, 2025 06:42Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza wazi masharti yake ya kufanya mazungumzo na nchi za Magharibi, huku ikisisitiza kutofanya mazungumzo yaliyosimama kwenye msingi wa mashinikizo na vitisho.
-
Iran yakosoa vikali uingiliaji wa nchi za Magharibi katika kazi za Baraza la Haki za Kibinadamu UN
Mar 19, 2025 00:45Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva amezikosoa vikali baadhi ya nchi za Magharibi kwa kutumia vibaya taasisi za Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa, nchi hizo zinataka kuingiza siasa katika masuala ya haki za binadamu dhidi ya Iran kwa kupuuza masuala ya kimsingi ya haki za binadamu ukiwemo mgogoro wa Palestina.