-
Madaktari wa Upasuaji wa Indonesia washangazwa na usahihi wa roboti za Iran
Mar 04, 2025 04:28Roboti za upasuaji aina ya Sina, zinazotengenezwa nchini Iran na kusambazwa katika hospitali za Indonesia kwa madhumuni ya upasuaji, zimewashangaza wataalamu wa matibabu nchini humo.
-
Baqaei: IAEA haipaswi kutoa maoni kwa mujibu wa matashi ya kisiasa
Mar 03, 2025 23:31Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: "Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) haupaswi kotoa maoni kwa kuzingatia mitazamo ya kisiasa."
-
Iran: Fedheha ya Zelensky nchini Marekani, kengele ya hatari ya kurejea ubabe wa karne ya 19
Mar 03, 2025 11:17Iran imesema mwenendo wa kudhalilisha wa Rais wa Marekani, Donald Trump dhidi ya mwenzake wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, katika Ikulu ya White House unapaswa kuwa "kengele ya hatari" ya kurejea kwenye zama za karne ya 19 za uonevu na utumiaji mabavu katika uhusiano wa kimataifa.
-
Malengo ya Iran ya kuwa na ushirikiano mzuri na majirani zake katika nyuga mbalimbali
Mar 03, 2025 06:45Majid Takht Ravanchi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na Masuala ya Kisiasa amesema kuhusu mikutano na mazungumzo aliyofanya na maafisa wa Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) au Imarati kwamba majirani wana nafasi maalumu katika sera za nje za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran inakabiliwa na muungano wa madola ya kinafiki
Mar 03, 2025 03:38Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema Jamhuri ya Kiislamu haina tatizo na mataifa mengine; lakini hata hivyo inakabiliwa na muungano mpana wa "madola ya kinafiki" yanayojaribu kuingilia mambo yake ya ndani na kuvuruga uhusiano wake wa nje.
-
Pezeshkian: Ramadhani iwe chachu ya kuimarika umoja wa Waislamu
Mar 03, 2025 03:38Rais Masoud Pezeshkian wa Iran sambamba na kuwapongeza viongozi na mataifa ya Kiislamu kwa mnasaba wa kuwadia mwezi mtukufu wa Ramadhani, ametoa mwito kwa nchi za Kiislamu kuutumia mwezi huu wa baraka kama chachu ya kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwao.
-
Bunge la Iran lapiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri wa Uchumi
Mar 02, 2025 09:16Wabunge katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) wamepiga kura ya kumuondoa katika wadhifa wake Waziri wa Masuala ya Uchumi na Fedha wa Jamhuri ya Kiislamu, Abdolnaser Hemmati wakati wa kikao cha kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.
-
Spika: Mataifa yanayotegemea usalama kutoka nje yatafeli
Mar 02, 2025 08:56Mohammad Baqer Qalibaf, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema mustakabali wa nchi zinazotegemea mataifa mengine kwa ajili ya kudhaminiwa usalama na maendeleo ni kufeli na kugonga mwamba.
-
Qalibaf awatakia kheri ya Ramadhani maspika wenzake katika nchi za Kiislamu
Mar 02, 2025 03:26Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf amewapongeza maspika wenzake katika nchi za Kiislamu kwa kuwasili mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Kamanda: Jeshi la Iran linabadilisha mbinu za kukabiliana na vitisho
Mar 01, 2025 23:39Kamanda mwandamizi wa Iran amesema Iran itabadilisha mbinu na mikakati yake ya kijeshi ili kukabiliana na vitisho vinavyobadilika. Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran, Brigedia Jenerali Alireza Sabahi-Fard, ameyasema hayo Jumamosi na kuongeza kuwa maadui na wavamizi hawawezi kufikia anga ya Iran.