-
Kan'ani: Kubadilika kwa watu na serikali huko Marekani si muhimu kwa Iran
Jul 22, 2024 22:56Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema mabadiliko ya serikali huko Marekani si muhimu na hayana taathira yoyote katika sera za kigeni za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi Muadhamu asisitiza juu ya ushirikiano wa bunge na rais kwa ajili ya kuunda serikali inayofaa kiutendaji
Jul 22, 2024 08:19Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameelezea matumaini yake kuwa kupitia ushirikiano wa Rais Mteule na Bunge, baraza la mawaziri lenye watu waaminifu na wachapakazi litaundwa kwa ajili ya kutatua matatizo ya nchi na wananchi.
-
Pezeshkian: Wanaoiwekea vikwazo Iran waliwapa maadui silaha za kemikali
Jul 22, 2024 07:58Rais mteule wa Iran ameyakosoa vikali madola ambayo yameiwekea vikwazo Jamhuri ya Kiislamu akisisitiza kuwa, mataifa hayo yana historia nyeusi kwa kupeana silaha zilizotumiwa dhidi ya taifa hili katika miaka ya 1980.
-
Iran na Sudan zarejesha uhusiano; balozi wa Iran Khartoum akabidhi hati za utambulisho
Jul 21, 2024 23:44Kiongozi wa Baraza la Utawala wa Mpito na Mkuu wa Majeshi ya Sudan, Abdul Fattah Al-Burhan, amepokea hati za utambulisho za balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Sudan, Hassan Shah Hosseini.
-
Kukabidhiwa madaraka serikali ya awamu ya 14 kwa njia ya amani na utulivu kamili
Jul 21, 2024 23:00Kukabidhiwa madaraka rais mpya wa Iran, ni moja ya dalili za wazi za mkondo wa kukabidhi madaraka kwa njia ya amani na utulivu katika Jamhuri ya Kiislamu ya Kiislamu ya Iran, jambo ambalo linachukuliwa kuwa mfano mzuri na wa kuigwa na hata na nchi zinazodai kutekeleza demokrasia.
-
Rais mteule wa Iran ashiriki katika kikao cha wazi cha Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge)
Jul 21, 2024 08:52Masoud Pezeshkian Rais mteule wa Iran leo ameshiriki katika kikao cha wazi cha Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) na kusisitiza kutatuliwa matatizo ya wananchi kupitia uratibu, maelewano na ushirikiano.
-
Kiongozi Muadhamu: Kufanikiwa Rais mpya wa Iran, ni mafanikio kwetu sote
Jul 21, 2024 07:33Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameiasa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) idumishe maingiliano yenye kujenga na uongozi wa Rais mteule wa Jamhuri ya Kiislamu, Masoud Pezeshkian na kusema kuwa, mafanikio ya Rais mpya wa Iran ya Kiislamu ni mafanikio ya taifa hili zima.
-
Iran yapongeza hukumu ya ICJ, yataka kura ya maoni kuamua mustakbali wa Palestina
Jul 20, 2024 23:04Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, njia bora zaidi ya kulipatia ufumbuzi suala la Palestina na kukomeshwa jinai za utawala haramu wa Israel, ni kufanyika kura ya maoni itakayowashirikisha Wapalestina wa ardhi zote za taifa hilo ili waamue mustakbali wao.
-
Marekani chimbuko kuu la matatizo Asia Magharibi
Jul 20, 2024 07:03Kaimu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amekosoa vikali maamuzi na hatua za mabavu na za upande mmoja zinazochukuliwa na Marekani katika masuala mbali mbali ya Asia Magharibi na kubainisha kwamba, hatua hizo ndio chimbuko kuu la matatizo yanayolikumba eneo hili.
-
Utayari wa Iran wa kushirikiana katika kuimarisha amani na usalama katika eneo
Jul 20, 2024 04:31Amir Saeid Iravani Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Iran iko tayari kushirikiana na nchi nyingine katika fremu ya Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai na Umoja wa Mataifa ili kukabiliana na changamoto za dharura na kuimarisha amani na usalama katika eneo.