-
Baada ya Iran kuapa kuwa itajibu mapigo makali, Trump asitisha mashambulizi dhidi ya miundombinu
Aug 02, 2026 13:15Rais wa Marekani Donald Trump amesema amefuta mashambulizi aliyotangaza kuwa yatafanywa dhidi ya Iran baada ya nchi za eneo kuomba yasitishwe wakati juhudi zinafanywa ili kufikia makubaliano, na kufuatia maonyo yaliyotolewa na Tehran kwamba uchokozi wowote mpya wa Marekani au Israel utakabiliwa na jibu la mapigo makali.
-
Abdel Bari Atwan: Makamanda wa jeshi la Marekani wanahofia kurudiwa "tajiriba ya Vietnam"
Aug 02, 2026 13:06Abdel Bari Atwan, mchambuzi mashuhuri katika Ulimwengu wa Kiarabu ameashiria jinsi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilivyojiandaa kutoa kipigo kikali dhidi ya uchokozi wowote, na hofu ya makamanda wa kijeshi wa Marekani ya kujirudia tajriba ya Vita vya Vietnam, na kutaja sababu tano zilizomfanya Trump arudi nyuma katika kutekeleza vitisho vyake.
-
Araqchi: Iran iko tayari kukabiliana na uvamizi wowote mpya wa Marekani
Aug 02, 2026 03:14Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi ameonya dhidi ya kitendo chochote kipya cha uvamizi cha Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, akisisitiza kwamba Tehran iko tayari kikamilifu kukabiliana na makosa yoyote kama hayo.
-
Kamanda Mkuu wa Iran: Nchi za kanda hii zinazotumika kama ngao ya Marekani 'zitateketea katika moto wa vita'
Aug 01, 2026 11:32Mkuu wa Kamandi Kuu ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Khatamul-Anbiya (SAW) amezionya nchi za kanda hii kuhusu kushirikiana na Marekani akisema: Nchi yoyote itakayotumika kama "ngao ya ulinzi" kwa Washington itaungua katika moto wa vita.
-
IRGC yazilenga na kuzisimamisha meli mbili za mafuta katika Lango la Hormuz
Aug 01, 2026 06:34Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) jana lilitangaza kuwa zimezishambulia meli mbili za mafuta katika Lango Bahari la Hormuz na kuzisimamisha baada ya kukiuka sheria na tahadhari ilizopewa.
-
Hatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Marekani si mchezaji mkuu tena Asia Magharibi
Jul 31, 2026 10:58Imamu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran, amesema Marekani si mchezaji mkuu tena katika eneo la Magharibi mwa Asia, akisisitiza kwamba: "Leo, kwa hatua za Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na mapambano yanayotokana na maarifa na imani ya wapiganaji wa Jeshi la Iran na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imefikia kiwango cha juu cha kujilinda ambacho kinamfanya adui asiwezi kuanza chochoko ya aina yoyote bila kupata jibu linalofaa."
-
Droni za Jeshi la Iran zashambulia vituo vya kimkakati vya Marekani nchini Kuwait
Jul 31, 2026 09:59Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limeshambulia vituo vya kimkakati vya jeshi la kigaidi la Marekani katika kambi ya Ahmed al-Jaber huko Kuwait kwa kutumia ndege zisizo na rubani zenye uharibifu mkubwa.
-
Baghaei amhoji Guterres; kwa nini unahepa kuwataja wavurugaji wawili wakuu wa sheria za kimataifa?
Jul 31, 2026 03:40Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria matamshi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kupuuzwa kwa sheria za kimataifa kwa namna inayotisha, na kumhutubu yeye kwa kumwambia: "Sasa ni wakati wa kutimiza jukumu lako zito na kusaidia kuzuia Umoja wa Mataifa na mfumo wa kanuni zake kutofikwa na hatima ya Jumuiya ya Mataifa."
-
Zaidi ya watu milioni 2 wavuka mipaka ya Iran kwa ajili ya Arubaini ya Imam Hussein (AS)
Jul 31, 2026 03:33Zaidi ya mazuwari milioni mbili wa Iran wamevuka salama mipaka ya nchi ili kuhudhuria shughuli ya kila mwaka ya Arubaini ya Imam Hussein, mojawapo ya mikusanyiko mikubwa zaidi ya kidini duniani, inayofanyika katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq.
-
Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran yaharibu ndege tatu za F-35 katika kambi ya Marekani huko Jordan
Jul 30, 2026 14:59Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limefanya mashambulizi ya makombora ya balestiki kwenye Kituo cha Anga cha Muwaffaq Salti kinachoendeshwa na jeshi la Marekani huko Azraq, nchini Jordan, na kuharibu ndege tatu za kivita za Marekani aina ya F-35 na kusababisha madhara makubwa kwa ndege nyingine tatu, katika operesheni ya kulipiza kisasi kwa shambulio la anga la Marekani lililoua watu watatu wa familia moja kwenye Kisiwa cha Qeshm nchini Iran.