-
Mapambano ya Watu wa Iran dhidi ya Madhalimu
Mar 31, 2026 04:51Swali muhimu zaidi ambalo limekuwa likiwashughulisha wachambuzi wengi na hata watumiaji wa mitandao ya kijamii siku hizi ni kuwa: "Je, Wairani wameweza vipi kusimama imara mbele ya nguvu mbili zenye silaha za nyuklia bila kuogopa wala kusalimu amri?"
-
Iran yakanusha kuwepo mazungumzo yoyote na Marekani
Mar 31, 2026 00:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei, amesisitiza kuwa Tehran haijafanya mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani, na amekanusha madai kwamba Jamhuri ya Kiislamu imekubali mapendekezo ya Washington, akieleza kauli hizo kuwa hazina msingi wowote.
-
Kamanda wa Kikosi cha Quds cha IRGC: Israel izoee “Mfumo Mpya wa Kikanda”
Mar 30, 2026 23:07Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Esmaeil Qaani, amesema kuwa utawala wa Israel unapaswa kuanza kuzoea “mfumo mpya wa nguvu katika kanda y Magharibi mwa Asia,” akisisitiza kwamba hatua zilizoratibiwa na washirika wa Iran katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) zimepunguza kwa kiasi kikubwa matarajio ya usalama ya Israel.
-
Awamu ya pili ya wimbi la 86 la Oparesheni Ahadi ya Kweli-4; ulipizaji kisasi dhidi ya maeneo ya viwanda ya adui
Mar 30, 2026 07:20Idara ya Uhusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imetoa taarifa ikitangaza kuwa jeshi hilo limetekeleza awamu ya pili ya wimbi la 86 la Oparesheni Ahadi ya Kweli-4 dhidi ya kitongoji cha viwanda cha Neot Hovav huko Beersheba kusini mwa ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina (Israel).
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu awashukuru wanazuoni wakuu na wananchi wa Iraq
Mar 30, 2026 01:55Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameshukuru na kuthamini misimamo ya msingi ya wanazuoni wakuu wa kidini na wananchi wa Iraq.
-
Admeri Irani awaonya Wamarekani: Manowari ya Lincoln ikija karibu, tutalipiza kisasi cha damu ya mashahidi wa Dena.
Mar 30, 2026 01:54Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewaonya Wamarekani akisema: "Mara tu manowari ya kubeba ndege ya Abraham Lincoln itakapokaribia eneo letu la ulengaji shabaha, tutalipiza kisasi cha damu ya mashahidi wa manowari ya Dena kwa kurusha aina mbalimbali ya makombora kutoka pwani hadi baharini."
-
Jeshi la Iran: Wanajeshi wa Marekani watageuzwa kuwa “Chakula cha Papa”
Mar 29, 2026 23:17Msemaji wa Kamandi ya Khatam al‑Anbia ya Jeshi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonya kuwa uvamizi wowote wa kijeshi wa Marekani kupitia nchi kavu au jaribio la kuikalia kwa mabavu ardhi ya Iran utamalizika kwa madhara makubwa, akisema askari wa Marekani watakumbana na maangamizi na hata kugeuka “chakula cha papa” katika Ghuba ya Uajemi.
-
Spika wa Bunge: Iran imekataa matakwa ya Marekani na Israel ya “Kujisalimisha,” Itapigana hadi ushindi
Mar 29, 2026 23:09Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema Iran haitakubali kamwe masharti ya kujisalimisha yanayotolewa na Marekani na Israel, na itaendelea kupigana hadi ipate ushindi.
-
Kwa nini jiografia inaipa Iran nafasi nzuri katika Lango-Bahari la Hormuz?
Mar 29, 2026 08:56Lango Bahari la Hormuz takriban limefungwa kwa wiki nne sasa na hivyo kupelekea soko la mafuta duniani kutumbukia katika mgogoro mkubwa wa nishati na wala haijulikani litafunguliwa lini.
-
Iran yaangusha ndege nyingine ya kivita aina ya F 16 ya adui
Mar 29, 2026 00:02Idara ya Uhusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imetangaza kwamba wimbi la 85 la Operesheni Ahadi ya Kweli 4 lilitekelezwa, kwa kushambulia viwanda kadhaa vikubwa vya adui na kuharibu ndege nyingine ya kivita ya F-16 ya adui.