-
Ghazizadeh Hashemi ajiondoa katika kinyang'anyiro cha urais wa Iran
Jun 26, 2024 23:30Amir-Hossein Ghazizadeh Hashemi, mmoja wa wagombea sita wa kiti cha rais ajaye wa Iran, amejiondoa katika kinyang'anyiro hicho. Uchaguzi huo wa kabla ya wakati wake unafanyika kesho Ijumaa tarehe 28 Juni, 2024.
-
Kani: Sera ya ujirani mwema ya Shahidi Raisi iliweka wazi sura mpya ya Iran
Jun 26, 2024 10:13Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa, sera kuu za Jamhuri ya Kiislamu zimejengeka katika msingi wa kuwa na ujirani mwema na kupanua mahusiano na majirani zake katika eneo.
-
Canada yazuia Wairani kushiriki uchaguzi wa rais wa Iran nchini humo
Jun 26, 2024 08:20Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran amesema Wairani walioko katika nchi za Canada na Saudi Arabia hawatapata fursa ya kushiriki uchaguzi wa rais wa mapema unaotazamiwa kufanyika Ijumaa ijayo.
-
Ushiriki wa kiwango cha juu zaidi; mkakati wa kudumu wa Kiongozi wa Mapinduzi kuhusu uchaguzi
Jun 26, 2024 05:48Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria uchaguzi muhimu sana wa siku ya Ijumaa (28 Juni), na kusisitizia ushiriki wa kiwango cha juu kabisa wa wananchi na kuwataka wananchi wa taifa hili kujitokeza katika vituo vya kupigia kura Ijumaa ya keshokutwa ili kumchagua Rais mpya.
-
Msisitizo wa Iran wa kuondoka bila masharti Marekani kutoka Syria
Jun 26, 2024 03:28Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, ni jambo la dharura kwa vikosi vya Marekani kuondoka kikamilifu, kwa haraka na bila masharti kutoka Syria na kwamba, hatua hiyo ni muhimu kwa ajili ya amani na utulivu wa nchi hiiyo ya Kiarabu.
-
Tehran, mwenyeji wa Jumuiya ya Mazungumzo ya Ushirikiano wa Asia (ACD).
Jun 25, 2024 22:47Kikao cha 19 cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Mazungumzo ya Ushirikiano wa Asia (ACD) kilifanyika Jumatatu hapa mjini Tehran chini ya uenyekiti wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi Muadhamu: Ushiriki mkubwa katika uchaguzi ni fahari kwa Iran, kiwewe kwa maadui
Jun 25, 2024 10:04Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema ushiriki mkubwa zaidi katika uchaguzi wa rais wa kabla ya wakati unatazamiwa kufanyika Juni 28, utalipa fahari taifa la Iran na kuwaghadhabisha maadui wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kiongozi Muadhamu akutana na wananchi katika sherehe za Sikukuu ya Eid Ghadir Khum
Jun 25, 2024 04:31Ayatullah Khamenei Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu leo amekutana na kuzungumza na maelfu ya wananchi katika sherehe ya maadhimisho ya Sikukuu ya Eid Ghadir Khum.
-
Vyombo vya habari vya nje 150 kuripoti uchaguzi wa Rais wa Iran
Jun 25, 2024 04:15Wizara ya Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa vyombo vya habari vya nje 150 kutoka nchi 31 vitaripoti zoezi la uchaguzi wa rais wa Iran utaofanyika Ijumaa ijayo Juni 28.
-
FAO: Iran kuzalisha zaidi ya tani milioni 20 za nafaka
Jun 25, 2024 04:15Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limetangaza kuwa, uzalishaji wa nafaka katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran utazidi tani milioni 20 mwaka huu.